< Zaburi 115 >

1 Sio kwetu, Yahwe, sio kwetu, bali kwa jina lako ulete heshima, kwa ajili ya uaminifu wa agano lako na uaminifu wako.
Not to us, Lord, not to us, but to you all glory should be given, because of your trustworthy love and faithfulness.
2 Kwa nini mataifa yalazimike kusema, “Yuko wapi Mungu wako?”
Why should the heathen nations ask, “Where is your God?”
3 Mungu wetu aliye mbinguni; hufanya chochote apendacho.
Our God is in heaven, and he does whatever he wants.
4 Sanamu za mataifa ni fedha na dhahabu, kazi ya mikono ya wanadamu.
Their idols are just things of silver and gold made by human hands.
5 Sanamu hizo zina vinywa, lakini haziongei; zina macho, lakini hazioni;
They have mouths, but can't speak. They have eyes, but can't see.
6 zina masikio, lakini hazisikii; zina pua lakini hazinusi.
They have ears, but can't hear. They have noses, but can't smell.
7 Sanamu hizo zina mikono, lakini hazishiki; zina miguu, lakini haziwezi kutembea; wala haziongei kutoka viywani mwao.
They have hands, but can't feel. They have feet, but can't walk. No sound comes from their throats.
8 Wale wanao zitengeneza wanafanana nazo, vile vile yeyote anaye amini katika hizo.
Those who make idols become just like them, and so does everyone who trusts in them.
9 Israeli, amini katika Yahwe; yeye ni msaada wako na ngao yako.
Israel, trust in the Lord! He is the one who helps you and protects you.
10 Nyumba ya Haruni, amini katika Yahwe; yeye ni msaada wako na ngao yako.
Descendants of Aaron, trust in the Lord! He is the one who helps you and protects you.
11 Ninyi mnao mheshumu Yahwe, mwamini yeye; yeye ni msaada wenu na ngao yenu.
Those who honor the Lord, trust in the Lord! He is the one who helps you and protects you.
12 Yahwe hutukumbuka sisi na atatubariki; ataibariki familia ya Israeli; atabariki familia ya Haruni.
The Lord keeps us in mind and will be good to us. He will bless Israel, he will bless the descendants of Aaron.
13 Atawabariki wale wanao muheshimu yeye, wote vijana na wazee.
The Lord will bless all those who worship him, whoever they are.
14 Yahwe na awaongeze ninyi zaidi na zaidi, ninyi pamoja na watoto wenu.
May the Lord be good to you, you and your children.
15 Yahwe na awabariki, aliyeziumba mbingu na nchi.
May you be blessed by the Lord who made heaven and earth.
16 Mbingu ni za Yahwe; lakini nchi amewapa wanadamu.
The heavens belong to the Lord, but he has given the earth to humankind.
17 Wafu hawamsifu Yahwe, wala wote washukao chini kwenye ukimya;
The dead do not praise the Lord, those who have gone down into the silence of the grave.
18 bali tutamtukuza Yahwe sasa na hata milele. Msifuni Yahwe.
But we the living will always praise the Lord. Praise the Lord!

< Zaburi 115 >