< Zaburi 115 >
1 Sio kwetu, Yahwe, sio kwetu, bali kwa jina lako ulete heshima, kwa ajili ya uaminifu wa agano lako na uaminifu wako.
Not to us, O Lord, not to us, but to your name give glory.
2 Kwa nini mataifa yalazimike kusema, “Yuko wapi Mungu wako?”
Give glory to your mercy and your truth, lest the Gentiles should say, “Where is their God?”
3 Mungu wetu aliye mbinguni; hufanya chochote apendacho.
But our God is in heaven. All things whatsoever that he has willed, he has done.
4 Sanamu za mataifa ni fedha na dhahabu, kazi ya mikono ya wanadamu.
The idols of the nations are silver and gold, the works of the hands of men.
5 Sanamu hizo zina vinywa, lakini haziongei; zina macho, lakini hazioni;
They have mouths, and do not speak; they have eyes, and do not see.
6 zina masikio, lakini hazisikii; zina pua lakini hazinusi.
They have ears, and do not hear; they have noses, and do not smell.
7 Sanamu hizo zina mikono, lakini hazishiki; zina miguu, lakini haziwezi kutembea; wala haziongei kutoka viywani mwao.
They have hands, and do not feel; they have feet, and do not walk. Neither will they cry out with their throat.
8 Wale wanao zitengeneza wanafanana nazo, vile vile yeyote anaye amini katika hizo.
Let those who make them become like them, along with all who trust in them.
9 Israeli, amini katika Yahwe; yeye ni msaada wako na ngao yako.
The house of Israel has hoped in the Lord. He is their helper and their protector.
10 Nyumba ya Haruni, amini katika Yahwe; yeye ni msaada wako na ngao yako.
The house of Aaron has hoped in the Lord. He is their helper and their protector.
11 Ninyi mnao mheshumu Yahwe, mwamini yeye; yeye ni msaada wenu na ngao yenu.
Those who fear the Lord have hoped in the Lord. He is their helper and their protector.
12 Yahwe hutukumbuka sisi na atatubariki; ataibariki familia ya Israeli; atabariki familia ya Haruni.
The Lord has been mindful of us, and he has blessed us. He has blessed the house of Israel. He has blessed the house of Aaron.
13 Atawabariki wale wanao muheshimu yeye, wote vijana na wazee.
He has blessed all who fear the Lord, the small with the great.
14 Yahwe na awaongeze ninyi zaidi na zaidi, ninyi pamoja na watoto wenu.
May the Lord add blessings upon you: upon you, and upon your sons.
15 Yahwe na awabariki, aliyeziumba mbingu na nchi.
Blessed are you by the Lord, who made heaven and earth.
16 Mbingu ni za Yahwe; lakini nchi amewapa wanadamu.
The heaven of heaven is for the Lord, but the earth he has given to the sons of men.
17 Wafu hawamsifu Yahwe, wala wote washukao chini kwenye ukimya;
The dead will not praise you, Lord, and neither will all those who descend into Hell. ()
18 bali tutamtukuza Yahwe sasa na hata milele. Msifuni Yahwe.
But we who live will bless the Lord, from this time forward, and even forever.