< Zaburi 115 >

1 Sio kwetu, Yahwe, sio kwetu, bali kwa jina lako ulete heshima, kwa ajili ya uaminifu wa agano lako na uaminifu wako.
Not to us, O Lord, not to us, but to your name let glory be given, because of your mercy and your unchanging faith.
2 Kwa nini mataifa yalazimike kusema, “Yuko wapi Mungu wako?”
Why may the nations say, Where is now their God?
3 Mungu wetu aliye mbinguni; hufanya chochote apendacho.
But our God is in heaven: he has done whatever was pleasing to him.
4 Sanamu za mataifa ni fedha na dhahabu, kazi ya mikono ya wanadamu.
Their images are silver and gold, the work of men's hands.
5 Sanamu hizo zina vinywa, lakini haziongei; zina macho, lakini hazioni;
They have mouths, but no voice; they have eyes, but they see not;
6 zina masikio, lakini hazisikii; zina pua lakini hazinusi.
They have ears, but no hearing; they have noses, but no sense of smell;
7 Sanamu hizo zina mikono, lakini hazishiki; zina miguu, lakini haziwezi kutembea; wala haziongei kutoka viywani mwao.
They have hands without feeling, and feet without power of walking; and no sound comes from their throat.
8 Wale wanao zitengeneza wanafanana nazo, vile vile yeyote anaye amini katika hizo.
Those who make them are like them; and so is everyone who puts his faith in them.
9 Israeli, amini katika Yahwe; yeye ni msaada wako na ngao yako.
O Israel, have faith in the Lord: he is their help and their breastplate.
10 Nyumba ya Haruni, amini katika Yahwe; yeye ni msaada wako na ngao yako.
O house of Aaron, have faith in the Lord: he is their help and their breastplate.
11 Ninyi mnao mheshumu Yahwe, mwamini yeye; yeye ni msaada wenu na ngao yenu.
You worshippers of the Lord, have faith in the Lord: he is their help and their breastplate.
12 Yahwe hutukumbuka sisi na atatubariki; ataibariki familia ya Israeli; atabariki familia ya Haruni.
The Lord has kept us in mind and will give us his blessing; he will send blessings on the house of Israel and on the house of Aaron.
13 Atawabariki wale wanao muheshimu yeye, wote vijana na wazee.
He will send blessings on the worshippers of the Lord, on the small and on the great.
14 Yahwe na awaongeze ninyi zaidi na zaidi, ninyi pamoja na watoto wenu.
May the Lord give you and your children still greater increase.
15 Yahwe na awabariki, aliyeziumba mbingu na nchi.
May you have the blessing of the Lord, who made heaven and earth.
16 Mbingu ni za Yahwe; lakini nchi amewapa wanadamu.
The heavens are the Lord's; but the earth he has given to the children of men.
17 Wafu hawamsifu Yahwe, wala wote washukao chini kwenye ukimya;
The dead do not give praise to the Lord; or those who go down to the underworld.
18 bali tutamtukuza Yahwe sasa na hata milele. Msifuni Yahwe.
But we will give praise to the Lord now and for ever. Praise be to the Lord.

< Zaburi 115 >