< Zaburi 114 >

1 Israeli ilipotoka Misri, na nyumba ya Yakobo toka kutoka katika wale watu wa kigeni,
When Israel went forth out of Egypt, the house of Jacob from a people of a strange language:
2 Yuda ilifanyika kuwa mahali pake patakatifu, Ufalme wa Israeli.
Judah became his sanctuary, [and] Israel his dominion.
3 Bahari iliona ikakimbia; Yordani ilirudi nyuma.
The sea beheld it, and fled: the Jordan was driven backward.
4 Milima iliruka kama kondoo waume, vilima viliruka kama wana-kondoo.
The mountains skipped like wethers, the hills like lambs.
5 Ewe Bahari kwa nini ulikimbia? Yordani kwa nini ulirudi nyuma?
What aileth thee, O sea, that thou fleest? thou, O Jordan, that thou art driven backward?
6 Milima, kwa nini uliruka kama kondoo waume? Enyi vilima wadogo, kwa nini mliruka kama wana-kondoo?
Ye mountains, that ye skip like wethers? ye hills, like lambs?
7 Tetemeka, ee nchi, mbele za Bwana, uweponi mwa Mungu wa Yakobo.
At the presence of the Lord tremble, O earth, at the presence of the God of Jacob;
8 Aligeuza mwamba kuwa ziwa la maji, jiwe gumu kuwa chemchem.
Who changeth the rock into a pool of water, the flint into a fountain of water.

< Zaburi 114 >