< Zaburi 114 >

1 Israeli ilipotoka Misri, na nyumba ya Yakobo toka kutoka katika wale watu wa kigeni,
When Israel went out of Egypt, the house of Jacob from a people of strange language;
2 Yuda ilifanyika kuwa mahali pake patakatifu, Ufalme wa Israeli.
Judah was his sanctuary, and Israel his dominion.
3 Bahari iliona ikakimbia; Yordani ilirudi nyuma.
The sea saw it, and fled: Jordan was driven back.
4 Milima iliruka kama kondoo waume, vilima viliruka kama wana-kondoo.
The mountains skipped like rams, and the little hills like lambs.
5 Ewe Bahari kwa nini ulikimbia? Yordani kwa nini ulirudi nyuma?
What ailed you, O you sea, that you fled? you Jordan, that you were driven back?
6 Milima, kwa nini uliruka kama kondoo waume? Enyi vilima wadogo, kwa nini mliruka kama wana-kondoo?
You mountains, that you skipped like rams; and you little hills, like lambs?
7 Tetemeka, ee nchi, mbele za Bwana, uweponi mwa Mungu wa Yakobo.
Tremble, you earth, at the presence of the Lord, at the presence of the God of Jacob;
8 Aligeuza mwamba kuwa ziwa la maji, jiwe gumu kuwa chemchem.
Which turned the rock into a standing water, the flint into a fountain of waters.

< Zaburi 114 >