< Zaburi 114 >

1 Israeli ilipotoka Misri, na nyumba ya Yakobo toka kutoka katika wale watu wa kigeni,
When Israel went out of Egypt, the house of Jacob from a barbarous people:
2 Yuda ilifanyika kuwa mahali pake patakatifu, Ufalme wa Israeli.
Judea made his sanctuary, Israel his dominion.
3 Bahari iliona ikakimbia; Yordani ilirudi nyuma.
The sea saw and fled: Jordan was turned back.
4 Milima iliruka kama kondoo waume, vilima viliruka kama wana-kondoo.
The mountains skipped like rams, and the hills like the lambs of the flock.
5 Ewe Bahari kwa nini ulikimbia? Yordani kwa nini ulirudi nyuma?
What ailed thee, O thou sea, that thou didst flee: and thou, O Jordan, that thou wast turned back?
6 Milima, kwa nini uliruka kama kondoo waume? Enyi vilima wadogo, kwa nini mliruka kama wana-kondoo?
Ye mountains, that ye skipped like rams, and ye hills, like lambs of the flock?
7 Tetemeka, ee nchi, mbele za Bwana, uweponi mwa Mungu wa Yakobo.
At the presence of the Lord the earth was moved, at the presence of the God of Jacob:
8 Aligeuza mwamba kuwa ziwa la maji, jiwe gumu kuwa chemchem.
Who turned the rock into pools of water, and the stony hill into fountains of waters.

< Zaburi 114 >