< Zaburi 113 >

1 Msifuni Yahwe. Msifuni yeye, enyi watumishi wa Yahwe; lisifuni jina la Yahwe.
alleluia laudate pueri Dominum laudate nomen Domini
2 Litukuzwe jina la Yahwe, tangu sasa na hata milele.
sit nomen Domini benedictum ex hoc nunc et usque in saeculum
3 Toka maawio ya jua hata machweo yake, Jina la Yahwe lazima lisifiwe.
a solis ortu usque ad occasum laudabile nomen Domini
4 Yahwe ameinuliwa juu ya mataifa yote, na utukufu wake wafika juu mbinguni.
excelsus super omnes gentes Dominus super caelos gloria eius
5 Ni nani aliye kama Yahwe Mungu wetu, aliye na kiti chake juu,
quis sicut Dominus Deus noster qui in altis habitat
6 atazamaye chini angani na duniani?
et humilia respicit in caelo et in terra
7 Humwinua maskini toka mavumbini na kumpandisha muhitaji kutoka jaani,
suscitans a terra inopem et de stercore erigens pauperem
8 ili amketishe pamoja na wakuu, pamoja na wakuu wa watu wake.
ut conlocet eum cum principibus cum principibus populi sui
9 Humpa watoto wanamke aliye tasa, humfanya yeye kuwa mama wa watoto mwenye furaha. Msifuni Yahwe!
qui habitare facit sterilem in domo matrem filiorum laetantem

< Zaburi 113 >