< Zaburi 113 >
1 Msifuni Yahwe. Msifuni yeye, enyi watumishi wa Yahwe; lisifuni jina la Yahwe.
Halleluja! Lobet, ihr Knechte des HERRN, lobet den Namen des HERRN!
2 Litukuzwe jina la Yahwe, tangu sasa na hata milele.
Gelobet sei des HERRN Name von nun an bis in Ewigkeit!
3 Toka maawio ya jua hata machweo yake, Jina la Yahwe lazima lisifiwe.
Vom Aufgang der Sonne bis zu ihrem Niedergang sei gelobet der Name des HERRN!
4 Yahwe ameinuliwa juu ya mataifa yote, na utukufu wake wafika juu mbinguni.
Der HERR ist hoch über alle Heiden; seine Ehre gehet, soweit der Himmel ist.
5 Ni nani aliye kama Yahwe Mungu wetu, aliye na kiti chake juu,
Wer ist, wie der HERR, unser Gott? Der sich so hoch gesetzt hat
6 atazamaye chini angani na duniani?
und auf das Niedrige siehet im Himmel und auf Erden;
7 Humwinua maskini toka mavumbini na kumpandisha muhitaji kutoka jaani,
der den Geringen aufrichtet aus dem Staube und erhöhet den Armen aus dem Kot,
8 ili amketishe pamoja na wakuu, pamoja na wakuu wa watu wake.
daß er ihn setze neben die Fürsten, neben die Fürsten seines Volks;
9 Humpa watoto wanamke aliye tasa, humfanya yeye kuwa mama wa watoto mwenye furaha. Msifuni Yahwe!
der die Unfruchtbare im Hause wohnen macht, daß sie eine fröhliche Kindermutter wird. Halleluja!