< Zaburi 113 >

1 Msifuni Yahwe. Msifuni yeye, enyi watumishi wa Yahwe; lisifuni jina la Yahwe.
Praise Yahweh - praise O servants of Yahweh praise [the] name of Yahweh.
2 Litukuzwe jina la Yahwe, tangu sasa na hata milele.
May it be [the] name of Yahweh blessed from now and until perpetuity.
3 Toka maawio ya jua hata machweo yake, Jina la Yahwe lazima lisifiwe.
From [the] rising of [the] sun to setting its [is] to be praised [the] name of Yahweh.
4 Yahwe ameinuliwa juu ya mataifa yote, na utukufu wake wafika juu mbinguni.
[is] exalted Over all nations - Yahweh [is] above the heavens glory his.
5 Ni nani aliye kama Yahwe Mungu wetu, aliye na kiti chake juu,
Who? [is] like Yahweh God our who is making high to sit.
6 atazamaye chini angani na duniani?
Who is making low to look on the heavens and on the earth.
7 Humwinua maskini toka mavumbini na kumpandisha muhitaji kutoka jaani,
[he is] raising From [the] dust [the] poor from [the] ash heap he lifts up [the] needy.
8 ili amketishe pamoja na wakuu, pamoja na wakuu wa watu wake.
To make [him] sit with noble [people] with [the] noble [people] of people his.
9 Humpa watoto wanamke aliye tasa, humfanya yeye kuwa mama wa watoto mwenye furaha. Msifuni Yahwe!
[he is] causes to dwell - [the] barren [woman] of The house [the] mother of the children joyful praise Yahweh.

< Zaburi 113 >