< Zaburi 113 >
1 Msifuni Yahwe. Msifuni yeye, enyi watumishi wa Yahwe; lisifuni jina la Yahwe.
Praise YAH! Praise, you servants of YHWH. Praise the Name of YHWH.
2 Litukuzwe jina la Yahwe, tangu sasa na hata milele.
The Name of YHWH is blessed, From now on, and for all time.
3 Toka maawio ya jua hata machweo yake, Jina la Yahwe lazima lisifiwe.
From the rising of the sun to its going in, The Name of YHWH [is] praised.
4 Yahwe ameinuliwa juu ya mataifa yote, na utukufu wake wafika juu mbinguni.
YHWH [is] high above all nations, His glory [is] above the heavens.
5 Ni nani aliye kama Yahwe Mungu wetu, aliye na kiti chake juu,
Who [is] as our God YHWH, He is exalting [Himself] to sit?
6 atazamaye chini angani na duniani?
He is humbling [Himself] to look On the heavens and on the earth.
7 Humwinua maskini toka mavumbini na kumpandisha muhitaji kutoka jaani,
He is raising up the poor from the dust, He exalts the needy from a dunghill.
8 ili amketishe pamoja na wakuu, pamoja na wakuu wa watu wake.
To cause [them] to sit with princes, With the princes of His people.
9 Humpa watoto wanamke aliye tasa, humfanya yeye kuwa mama wa watoto mwenye furaha. Msifuni Yahwe!
Causing the barren one of the house to sit, A joyful mother of sons; praise YAH!