< Zaburi 113 >

1 Msifuni Yahwe. Msifuni yeye, enyi watumishi wa Yahwe; lisifuni jina la Yahwe.
Praise the Lord! Praise him, servants of the Lord! Praise the Lord's as he is!
2 Litukuzwe jina la Yahwe, tangu sasa na hata milele.
Let the Lord's nature be praised, now and forever.
3 Toka maawio ya jua hata machweo yake, Jina la Yahwe lazima lisifiwe.
Let everyone everywhere, from the east to the west, praise the Lord as he is!
4 Yahwe ameinuliwa juu ya mataifa yote, na utukufu wake wafika juu mbinguni.
The Lord rules supreme over all nations; his glory extends higher than the heavens.
5 Ni nani aliye kama Yahwe Mungu wetu, aliye na kiti chake juu,
Who is like the Lord our God? He is the one who lives on high, seated on his throne.
6 atazamaye chini angani na duniani?
He has to stoop low to look down on the heavens and the earth.
7 Humwinua maskini toka mavumbini na kumpandisha muhitaji kutoka jaani,
He helps the poor up from the dust; he lifts the needy from the dump.
8 ili amketishe pamoja na wakuu, pamoja na wakuu wa watu wake.
He gives them positions of honor together important leaders, with leaders of his own people.
9 Humpa watoto wanamke aliye tasa, humfanya yeye kuwa mama wa watoto mwenye furaha. Msifuni Yahwe!
He makes the childless woman happy in her home by giving her children. Praise the Lord!

< Zaburi 113 >