< Zaburi 113 >

1 Msifuni Yahwe. Msifuni yeye, enyi watumishi wa Yahwe; lisifuni jina la Yahwe.
Alleluia. Praise the Lord, you servants [of his], praise, the name of the Lord.
2 Litukuzwe jina la Yahwe, tangu sasa na hata milele.
Let the name of the Lord be blessed, from this present time and for ever.
3 Toka maawio ya jua hata machweo yake, Jina la Yahwe lazima lisifiwe.
From the rising of the sun to his setting, the name of the Lord is to be praised.
4 Yahwe ameinuliwa juu ya mataifa yote, na utukufu wake wafika juu mbinguni.
The Lord is high above all the nations; his glory is above the heavens.
5 Ni nani aliye kama Yahwe Mungu wetu, aliye na kiti chake juu,
Who is as the Lord our God? who dwells in the high places,
6 atazamaye chini angani na duniani?
and [yet] looks upon the low things in heaven, and on the earth:
7 Humwinua maskini toka mavumbini na kumpandisha muhitaji kutoka jaani,
who lifts up the poor from the earth, and raises up the needy from the dunghill;
8 ili amketishe pamoja na wakuu, pamoja na wakuu wa watu wake.
to set him with princes, [even] with the princes of his people:
9 Humpa watoto wanamke aliye tasa, humfanya yeye kuwa mama wa watoto mwenye furaha. Msifuni Yahwe!
who settles the barren [woman] in a house, [as] a mother rejoicing over children.

< Zaburi 113 >