< Zaburi 113 >
1 Msifuni Yahwe. Msifuni yeye, enyi watumishi wa Yahwe; lisifuni jina la Yahwe.
Hallelujah! Give praise, O servants of the LORD; praise the name of the LORD.
2 Litukuzwe jina la Yahwe, tangu sasa na hata milele.
Blessed be the name of the LORD both now and forevermore.
3 Toka maawio ya jua hata machweo yake, Jina la Yahwe lazima lisifiwe.
From where the sun rises to where it sets, the name of the LORD is praised.
4 Yahwe ameinuliwa juu ya mataifa yote, na utukufu wake wafika juu mbinguni.
The LORD is exalted over all the nations, His glory above the heavens.
5 Ni nani aliye kama Yahwe Mungu wetu, aliye na kiti chake juu,
Who is like the LORD our God, the One enthroned on high?
6 atazamaye chini angani na duniani?
He humbles Himself to behold the heavens and the earth.
7 Humwinua maskini toka mavumbini na kumpandisha muhitaji kutoka jaani,
He raises the poor from the dust and lifts the needy from the dump
8 ili amketishe pamoja na wakuu, pamoja na wakuu wa watu wake.
to seat them with nobles, with the princes of His people.
9 Humpa watoto wanamke aliye tasa, humfanya yeye kuwa mama wa watoto mwenye furaha. Msifuni Yahwe!
He settles the barren woman in her home as a joyful mother to her children. Hallelujah!