< Zaburi 112 >

1 Msifuni Yahwe. Amebarikiwa mtu yule anaye mtii Yahwe, apendezwaye sana na amri zake.
Msifuni Bwana. Heri mtu yule amchaye Bwana, mtu yule apendezwaye sana na amri zake.
2 Kizazi chake kitakuwa ni chenye nguvu duniani; kizazi cha mcha Mungu kitabarikiwa.
Watoto wake watakuwa wenye uwezo katika nchi, kizazi cha watu waadilifu kitabarikiwa.
3 Nyumbani mwake mna utajiri na mali; na haki yake itadumu milele.
Nyumbani mwake kuna mali na utajiri, haki yake hudumu milele.
4 Nuru huangazia gizani kwa ajili ya mtu mcha Mungu; yeye ni wa fadhili, huruma, na haki.
Hata gizani nuru humzukia mtu mwadilifu, yule mwenye rehema, huruma na haki.
5 Heri atendaye fadhili na kukopesha, afanyaye mambo yake kwa uaminifu.
Mema yatamjia mtu yule aliye mkarimu na mwenye kukopesha bila riba, anayefanya mambo yake kwa haki.
6 Kwa maana hataondoshwa kamwe; mwenye haki atakumbukwa milele.
Hakika hatatikisika kamwe, mtu mwenye haki atakumbukwa milele.
7 Haogopi habari mbaya; ni jasiri, akimtumainia Yahwe.
Hataogopa habari mbaya, moyo wake ni thabiti, ukimtegemea Bwana.
8 Moyo wake ni mtulivu, hana woga, mpaka aonapo ushindi dhidi ya watesi wake.
Moyo wake ni salama, hatakuwa na hofu, mwishoni ataona ushindi dhidi ya adui zake.
9 Huwapa masikini kwa ukarimu; haki yake yadumu milele; atainuliwa kwa heshima.
Ametawanya vipawa vyake kwa ukarimu akawapa maskini; haki yake hudumu milele; pembe yake itatukuzwa kwa heshima.
10 Mtu mwovu ataona haya na kukasirika; atasaga meno yake na kuyeyuka; tamaa ya wasio haki itapotea.
Mtu mwovu ataona na kuchukizwa, atasaga meno yake na kutoweka, kutamani kwa mtu mwovu kutaishia patupu.

< Zaburi 112 >