< Zaburi 111 >
1 Msifuni Yahwe. Nitamshukuru Yahwe kwa moyo wangu wote katikati ya kusanyiko la wanye haki, na katika mkutano.
Louez Jah. Je célébrerai l’Éternel de tout mon cœur, dans la compagnie des hommes droits et dans l’assemblée.
2 Kazi za Yahwe ni kuu, zikisubiriwa na wale wazitamanio.
Les œuvres de l’Éternel sont grandes, elles sont recherchées de tous ceux qui y prennent plaisir;
3 Kazi yake ni adhama na utukufu, na haki yake yadumu milele.
Son œuvre est glorieuse et magnifique, et sa justice demeure à perpétuité.
4 Hufanya mambo makuu ambayo yatakumbukwa; Yahwe ni mwenye huruma na neema.
Il a établi un mémorial de ses merveilles. L’Éternel est plein de grâce et miséricordieux;
5 Huwapa chakula wafuasi wake waaminifu. Siku zote atalikumbuka agano lake.
Il donne de la nourriture à ceux qui le craignent; il se souvient à toujours de son alliance;
6 Alionesha uweza wa kazi zake kwa watu wake kwa kuwapa urithi wa mataifa.
Il a montré à son peuple la puissance de ses œuvres, pour leur donner l’héritage des nations.
7 Kazi za mikono yake ni za kuaminika na haki; maagizo yake yote ni ya kuaminika.
Les œuvres de ses mains sont vérité et jugement; tous ses préceptes sont sûrs,
8 Yamethibitika milele, yamefanywa katika uaminifu na vizuri.
Maintenus à perpétuité, pour toujours, faits avec vérité et droiture.
9 Aliwapa ushindi watu wake; aliliteuwa agano lake milele; jina lake ni takatifu na lakutisha.
Il a envoyé la rédemption à son peuple; il a commandé son alliance pour toujours. Son nom est saint et terrible.
10 Kumcha Yahwe ni mwanzo wa hekima; wale washikao maagizo yake wana uelewa mzuri. Sifa yake yadumu milele.
La crainte de l’Éternel est le commencement de la sagesse; tous ceux qui pratiquent [ses préceptes] auront une bonne intelligence. Sa louange demeure à perpétuité.