< Zaburi 111 >

1 Msifuni Yahwe. Nitamshukuru Yahwe kwa moyo wangu wote katikati ya kusanyiko la wanye haki, na katika mkutano.
Louez Yah! Je rendrai grâce à Yahvé de tout mon cœur, dans le conseil des hommes intègres et dans l'assemblée.
2 Kazi za Yahwe ni kuu, zikisubiriwa na wale wazitamanio.
Les œuvres de Yahvé sont grandes, réfléchis par tous ceux qui les apprécient.
3 Kazi yake ni adhama na utukufu, na haki yake yadumu milele.
Son œuvre est honneur et majesté. Sa justice est éternelle.
4 Hufanya mambo makuu ambayo yatakumbukwa; Yahwe ni mwenye huruma na neema.
Il a fait en sorte qu'on se souvienne de ses merveilles. Yahvé est gracieux et miséricordieux.
5 Huwapa chakula wafuasi wake waaminifu. Siku zote atalikumbuka agano lake.
Il a donné de la nourriture à ceux qui le craignent. Il se souvient toujours de son engagement.
6 Alionesha uweza wa kazi zake kwa watu wake kwa kuwapa urithi wa mataifa.
Il a montré à son peuple la puissance de ses œuvres, en leur donnant l'héritage des nations.
7 Kazi za mikono yake ni za kuaminika na haki; maagizo yake yote ni ya kuaminika.
Les œuvres de ses mains sont la vérité et la justice. Tous ses préceptes sont sûrs.
8 Yamethibitika milele, yamefanywa katika uaminifu na vizuri.
Ils sont établis pour toujours et à jamais. Ils sont faits dans la vérité et la droiture.
9 Aliwapa ushindi watu wake; aliliteuwa agano lake milele; jina lake ni takatifu na lakutisha.
Il a envoyé la rédemption à son peuple. Il a établi son alliance pour toujours. Son nom est saint et impressionnant!
10 Kumcha Yahwe ni mwanzo wa hekima; wale washikao maagizo yake wana uelewa mzuri. Sifa yake yadumu milele.
La crainte de Yahvé est le commencement de la sagesse. Tous ceux qui font son travail ont une bonne compréhension. Sa louange est éternelle!

< Zaburi 111 >