< Zaburi 111 >
1 Msifuni Yahwe. Nitamshukuru Yahwe kwa moyo wangu wote katikati ya kusanyiko la wanye haki, na katika mkutano.
Praise ye Jah! I thank Jehovah with the whole heart, In the secret meeting of the upright, And of the company.
2 Kazi za Yahwe ni kuu, zikisubiriwa na wale wazitamanio.
Great [are] the works of Jehovah, Sought out by all desiring them.
3 Kazi yake ni adhama na utukufu, na haki yake yadumu milele.
Honourable and majestic is His work, And His righteousness is standing for ever.
4 Hufanya mambo makuu ambayo yatakumbukwa; Yahwe ni mwenye huruma na neema.
A memorial He hath made of His wonders, Gracious and merciful [is] Jehovah.
5 Huwapa chakula wafuasi wake waaminifu. Siku zote atalikumbuka agano lake.
Prey He hath given to those fearing Him, He remembereth to the age His covenant.
6 Alionesha uweza wa kazi zake kwa watu wake kwa kuwapa urithi wa mataifa.
The power of His works He hath declared to His people, To give to them the inheritance of nations.
7 Kazi za mikono yake ni za kuaminika na haki; maagizo yake yote ni ya kuaminika.
The works of His hands [are] true and just, Stedfast [are] all His appointments.
8 Yamethibitika milele, yamefanywa katika uaminifu na vizuri.
They are sustained for ever to the age. They are made in truth and uprightness.
9 Aliwapa ushindi watu wake; aliliteuwa agano lake milele; jina lake ni takatifu na lakutisha.
Redemption He hath sent to His people, He hath appointed to the age His covenant, Holy and fearful [is] His name.
10 Kumcha Yahwe ni mwanzo wa hekima; wale washikao maagizo yake wana uelewa mzuri. Sifa yake yadumu milele.
The beginning of wisdom [is] fear of Jehovah, Good understanding have all doing them, His praise [is] standing for ever!