< Zaburi 111 >

1 Msifuni Yahwe. Nitamshukuru Yahwe kwa moyo wangu wote katikati ya kusanyiko la wanye haki, na katika mkutano.
Praise ye the LORD. I will praise the LORD with [my] whole heart, in the assembly of the upright, and [in] the congregation.
2 Kazi za Yahwe ni kuu, zikisubiriwa na wale wazitamanio.
The works of the LORD [are] great, sought out by all them that have pleasure in them.
3 Kazi yake ni adhama na utukufu, na haki yake yadumu milele.
His work [is] honorable and glorious: and his righteousness endureth for ever.
4 Hufanya mambo makuu ambayo yatakumbukwa; Yahwe ni mwenye huruma na neema.
He hath made his wonderful works to be remembered: the LORD [is] gracious and full of compassion.
5 Huwapa chakula wafuasi wake waaminifu. Siku zote atalikumbuka agano lake.
He hath given food to them that fear him: he will ever be mindful of his covenant.
6 Alionesha uweza wa kazi zake kwa watu wake kwa kuwapa urithi wa mataifa.
He hath shown his people the power of his works, that he may give them the heritage of the heathen.
7 Kazi za mikono yake ni za kuaminika na haki; maagizo yake yote ni ya kuaminika.
The works of his hands [are] verity and judgment; all his commandments [are] sure.
8 Yamethibitika milele, yamefanywa katika uaminifu na vizuri.
They stand fast for ever and ever, [and are] done in truth and uprightness.
9 Aliwapa ushindi watu wake; aliliteuwa agano lake milele; jina lake ni takatifu na lakutisha.
He sent redemption to his people: he hath commanded his covenant for ever: holy and reverend [is] his name.
10 Kumcha Yahwe ni mwanzo wa hekima; wale washikao maagizo yake wana uelewa mzuri. Sifa yake yadumu milele.
The fear of the LORD [is] the beginning of wisdom: a good understanding have all they that do [his commandments]: his praise endureth for ever.

< Zaburi 111 >