< Zaburi 111 >

1 Msifuni Yahwe. Nitamshukuru Yahwe kwa moyo wangu wote katikati ya kusanyiko la wanye haki, na katika mkutano.
Praise Yahweh. I will give thanks to Yahweh with my whole heart in the assembly of the upright, in their gathering.
2 Kazi za Yahwe ni kuu, zikisubiriwa na wale wazitamanio.
The works of Yahweh are great, eagerly awaited by all those who desire them.
3 Kazi yake ni adhama na utukufu, na haki yake yadumu milele.
His work is majestic and glorious, and his righteousness endures forever.
4 Hufanya mambo makuu ambayo yatakumbukwa; Yahwe ni mwenye huruma na neema.
He does wonderful things that will be remembered; Yahweh is gracious and merciful.
5 Huwapa chakula wafuasi wake waaminifu. Siku zote atalikumbuka agano lake.
He gives food to his faithful followers. He will always call to mind his covenant.
6 Alionesha uweza wa kazi zake kwa watu wake kwa kuwapa urithi wa mataifa.
He showed his powerful works to his people in giving them the inheritance of the nations.
7 Kazi za mikono yake ni za kuaminika na haki; maagizo yake yote ni ya kuaminika.
The works of his hands are trustworthy and just; all his instructions are reliable.
8 Yamethibitika milele, yamefanywa katika uaminifu na vizuri.
They are established forever, to be observed faithfully and properly.
9 Aliwapa ushindi watu wake; aliliteuwa agano lake milele; jina lake ni takatifu na lakutisha.
He gave victory to his people; he ordained his covenant forever; holy and awesome is his name.
10 Kumcha Yahwe ni mwanzo wa hekima; wale washikao maagizo yake wana uelewa mzuri. Sifa yake yadumu milele.
To honor Yahweh is the beginning of wisdom; those who carry out his instructions have good understanding. His praise endures forever.

< Zaburi 111 >