< Zaburi 111 >

1 Msifuni Yahwe. Nitamshukuru Yahwe kwa moyo wangu wote katikati ya kusanyiko la wanye haki, na katika mkutano.
Hallelujah. I will give thanks unto the LORD with my whole heart, in the council of the upright, and in the congregation.
2 Kazi za Yahwe ni kuu, zikisubiriwa na wale wazitamanio.
The works of the LORD are great, sought out of all them that have delight therein.
3 Kazi yake ni adhama na utukufu, na haki yake yadumu milele.
His work is glory and majesty; and His righteousness endureth for ever.
4 Hufanya mambo makuu ambayo yatakumbukwa; Yahwe ni mwenye huruma na neema.
He hath made a memorial for His wonderful works; the LORD is gracious and full of compassion.
5 Huwapa chakula wafuasi wake waaminifu. Siku zote atalikumbuka agano lake.
He hath given food unto them that fear Him; He will ever be mindful of His covenant.
6 Alionesha uweza wa kazi zake kwa watu wake kwa kuwapa urithi wa mataifa.
He hath declared to His people the power of His works, in giving them the heritage of the nations.
7 Kazi za mikono yake ni za kuaminika na haki; maagizo yake yote ni ya kuaminika.
The works of His hands are truth and justice; all His precepts are sure.
8 Yamethibitika milele, yamefanywa katika uaminifu na vizuri.
They are established for ever and ever, they are done in truth and uprightness.
9 Aliwapa ushindi watu wake; aliliteuwa agano lake milele; jina lake ni takatifu na lakutisha.
He hath sent redemption unto His people; He hath commanded His covenant for ever; Holy and awful is His name.
10 Kumcha Yahwe ni mwanzo wa hekima; wale washikao maagizo yake wana uelewa mzuri. Sifa yake yadumu milele.
The fear of the LORD is the beginning of wisdom; a good understanding have all they that do thereafter; His praise endureth for ever.

< Zaburi 111 >