< Zaburi 111 >
1 Msifuni Yahwe. Nitamshukuru Yahwe kwa moyo wangu wote katikati ya kusanyiko la wanye haki, na katika mkutano.
Praise ye the Lord. I will prayse the Lord with my whole heart in the assemblie and Congregation of the iust.
2 Kazi za Yahwe ni kuu, zikisubiriwa na wale wazitamanio.
The workes of the Lord are great, and ought to be sought out of al them that loue them.
3 Kazi yake ni adhama na utukufu, na haki yake yadumu milele.
His worke is beautifull and glorious, and his righteousnesse endureth for euer.
4 Hufanya mambo makuu ambayo yatakumbukwa; Yahwe ni mwenye huruma na neema.
He hath made his wonderfull workes to be had in remembrance: the Lord is mercifull and full of compassion.
5 Huwapa chakula wafuasi wake waaminifu. Siku zote atalikumbuka agano lake.
He hath giuen a portion vnto them that feare him: he wil euer be mindfull of his couenant.
6 Alionesha uweza wa kazi zake kwa watu wake kwa kuwapa urithi wa mataifa.
He hath shewed to his people the power of his workes in giuing vnto them the heritage of the heathen.
7 Kazi za mikono yake ni za kuaminika na haki; maagizo yake yote ni ya kuaminika.
The workes of his handes are trueth and iudgement: all his statutes are true.
8 Yamethibitika milele, yamefanywa katika uaminifu na vizuri.
They are stablished for euer and euer, and are done in trueth and equitie.
9 Aliwapa ushindi watu wake; aliliteuwa agano lake milele; jina lake ni takatifu na lakutisha.
He sent redemption vnto his people: he hath commanded his couenant for euer: holy and fearefull is his Name.
10 Kumcha Yahwe ni mwanzo wa hekima; wale washikao maagizo yake wana uelewa mzuri. Sifa yake yadumu milele.
The beginning of wisedome is the feare of the Lord: all they that obserue them, haue good vnderstanding: his praise endureth for euer.