< Zaburi 111 >
1 Msifuni Yahwe. Nitamshukuru Yahwe kwa moyo wangu wote katikati ya kusanyiko la wanye haki, na katika mkutano.
I will praise thee, O Lord, with my whole heart; in the council of the just: and in the congregation.
2 Kazi za Yahwe ni kuu, zikisubiriwa na wale wazitamanio.
Great are the works of the Lord: sought out according to all his wills.
3 Kazi yake ni adhama na utukufu, na haki yake yadumu milele.
His work is praise and magnificence: and his justice continueth for ever and ever.
4 Hufanya mambo makuu ambayo yatakumbukwa; Yahwe ni mwenye huruma na neema.
He hath made a remembrance of his wonderful works, being a merciful and gracious Lord:
5 Huwapa chakula wafuasi wake waaminifu. Siku zote atalikumbuka agano lake.
He hath given food to them that fear him. He will be mindful for ever of his covenant:
6 Alionesha uweza wa kazi zake kwa watu wake kwa kuwapa urithi wa mataifa.
He will shew forth to his people the power of his works.
7 Kazi za mikono yake ni za kuaminika na haki; maagizo yake yote ni ya kuaminika.
That he may give them the inheritance of the Gentiles: the works of his hands are truth and judgment.
8 Yamethibitika milele, yamefanywa katika uaminifu na vizuri.
All his commandments are faithful: confirmed for ever and ever, made in truth and equity.
9 Aliwapa ushindi watu wake; aliliteuwa agano lake milele; jina lake ni takatifu na lakutisha.
He hath sent redemption to his people: he hath commanded his covenant for ever. Holy and terrible is his name:
10 Kumcha Yahwe ni mwanzo wa hekima; wale washikao maagizo yake wana uelewa mzuri. Sifa yake yadumu milele.
The fear of the Lord is the beginning of wisdom. A good understanding to all that do it: his praise continueth for ever and ever.