< Zaburi 111 >
1 Msifuni Yahwe. Nitamshukuru Yahwe kwa moyo wangu wote katikati ya kusanyiko la wanye haki, na katika mkutano.
Alleluia. I will confess to you, O Lord, with my whole heart, in the council of the just and in the congregation.
2 Kazi za Yahwe ni kuu, zikisubiriwa na wale wazitamanio.
Great are the works of the Lord, exquisite in all his intentions.
3 Kazi yake ni adhama na utukufu, na haki yake yadumu milele.
Confession and magnificence are his work. And his justice remains from age to age.
4 Hufanya mambo makuu ambayo yatakumbukwa; Yahwe ni mwenye huruma na neema.
He has created a memorial to his wonders; he is a merciful and compassionate Lord.
5 Huwapa chakula wafuasi wake waaminifu. Siku zote atalikumbuka agano lake.
He has given food to those who fear him. He will be mindful of his covenant in every age.
6 Alionesha uweza wa kazi zake kwa watu wake kwa kuwapa urithi wa mataifa.
He will announce the virtue of his works to his people,
7 Kazi za mikono yake ni za kuaminika na haki; maagizo yake yote ni ya kuaminika.
so that he may give them the inheritance of the nations. The works of his hands are truth and judgment.
8 Yamethibitika milele, yamefanywa katika uaminifu na vizuri.
All his commands are faithful: confirmed from age to age, created in truth and fairness.
9 Aliwapa ushindi watu wake; aliliteuwa agano lake milele; jina lake ni takatifu na lakutisha.
He has sent redemption upon his people. He has commanded his covenant for all eternity. Holy and terrible is his name.
10 Kumcha Yahwe ni mwanzo wa hekima; wale washikao maagizo yake wana uelewa mzuri. Sifa yake yadumu milele.
The fear of the Lord is the beginning of wisdom. A good understanding is for all who do it. His praise remains from age to age.