< Zaburi 111 >

1 Msifuni Yahwe. Nitamshukuru Yahwe kwa moyo wangu wote katikati ya kusanyiko la wanye haki, na katika mkutano.
Let the Lord be praised. I will give praise to the Lord with all my heart, among the upright, and in the meeting of the people.
2 Kazi za Yahwe ni kuu, zikisubiriwa na wale wazitamanio.
The works of the Lord are great, searched out by all those who have delight in them.
3 Kazi yake ni adhama na utukufu, na haki yake yadumu milele.
His work is full of honour and glory; and his righteousness is unchanging for ever.
4 Hufanya mambo makuu ambayo yatakumbukwa; Yahwe ni mwenye huruma na neema.
Certain for ever is the memory of his wonders: the Lord is full of pity and mercy.
5 Huwapa chakula wafuasi wake waaminifu. Siku zote atalikumbuka agano lake.
He has given food to his worshippers; he will keep his agreement in mind for ever.
6 Alionesha uweza wa kazi zake kwa watu wake kwa kuwapa urithi wa mataifa.
He has made clear to his people the power of his works, giving them the heritage of the nations.
7 Kazi za mikono yake ni za kuaminika na haki; maagizo yake yote ni ya kuaminika.
The works of his hands are faith and righteousness; all his laws are unchanging.
8 Yamethibitika milele, yamefanywa katika uaminifu na vizuri.
They are fixed for ever and ever, they are done in faith and righteousness.
9 Aliwapa ushindi watu wake; aliliteuwa agano lake milele; jina lake ni takatifu na lakutisha.
He has sent salvation to his people; he has given his word for ever: holy is his name and greatly to be feared.
10 Kumcha Yahwe ni mwanzo wa hekima; wale washikao maagizo yake wana uelewa mzuri. Sifa yake yadumu milele.
The fear of the Lord is the best part of wisdom: all those who keep his laws are wise: his praise is eternal.

< Zaburi 111 >