< Zaburi 111 >
1 Msifuni Yahwe. Nitamshukuru Yahwe kwa moyo wangu wote katikati ya kusanyiko la wanye haki, na katika mkutano.
Halleluja! jeg takker HERREN af hele mit Hjerte i Oprigtiges Kreds og Menighed!
2 Kazi za Yahwe ni kuu, zikisubiriwa na wale wazitamanio.
Store er HERRENS Gerninger, gennemtænkte til Bunds.
3 Kazi yake ni adhama na utukufu, na haki yake yadumu milele.
Hans Værk er Højhed og Herlighed, hans Retfærd bliver til evig Tid.
4 Hufanya mambo makuu ambayo yatakumbukwa; Yahwe ni mwenye huruma na neema.
Han har sørget for, at hans Undere mindes, naadig og barmhjertig er HERREN.
5 Huwapa chakula wafuasi wake waaminifu. Siku zote atalikumbuka agano lake.
Dem, der frygter ham, giver han Føde, han kommer for evigt sin Pagt i Hu.
6 Alionesha uweza wa kazi zake kwa watu wake kwa kuwapa urithi wa mataifa.
Han viste sit Folk sine vældige Gerninger, da han gav dem Folkenes Eje.
7 Kazi za mikono yake ni za kuaminika na haki; maagizo yake yote ni ya kuaminika.
Hans Hænders Værk er Sandhed og Ret, man kan lide paa alle hans Bud;
8 Yamethibitika milele, yamefanywa katika uaminifu na vizuri.
de staar i al Evighed fast, udført i Sandhed og Retsind.
9 Aliwapa ushindi watu wake; aliliteuwa agano lake milele; jina lake ni takatifu na lakutisha.
Han sendte sit Folk Udløsning, stifted sin Pagt for evigt. Helligt og frygteligt er hans Navn.
10 Kumcha Yahwe ni mwanzo wa hekima; wale washikao maagizo yake wana uelewa mzuri. Sifa yake yadumu milele.
HERRENS Frygt er Visdoms Begyndelse; forstandig er hver, som øver den. Evigt varer hans Pris!