< Zaburi 111 >
1 Msifuni Yahwe. Nitamshukuru Yahwe kwa moyo wangu wote katikati ya kusanyiko la wanye haki, na katika mkutano.
阿肋路亞。在義人的集會和團聚中,我要全心讚頌上主。
2 Kazi za Yahwe ni kuu, zikisubiriwa na wale wazitamanio.
上主的化工確實偉大,凡喜愛祂的必須究察。
3 Kazi yake ni adhama na utukufu, na haki yake yadumu milele.
上主的作為輝煌,上主的正義常存。
4 Hufanya mambo makuu ambayo yatakumbukwa; Yahwe ni mwenye huruma na neema.
上主的奇蹟不可遺忘;上主實在是慈愛而溫良。
5 Huwapa chakula wafuasi wake waaminifu. Siku zote atalikumbuka agano lake.
上主賜給敬愛祂的人食物,上主永遠懷念自己的盟約。
6 Alionesha uweza wa kazi zake kwa watu wake kwa kuwapa urithi wa mataifa.
祂將偉業的異能啟示給選民,把外邦人的產業賞賜給他們。
7 Kazi za mikono yake ni za kuaminika na haki; maagizo yake yote ni ya kuaminika.
上主所行的是真誠正義;上主的一切規誡堅定不移。
8 Yamethibitika milele, yamefanywa katika uaminifu na vizuri.
為萬世萬代永遠立定,全是基於真理和公正。
9 Aliwapa ushindi watu wake; aliliteuwa agano lake milele; jina lake ni takatifu na lakutisha.
祂速來救贖祂的百姓,永遠立定了祂的約盟;祂的名是神聖而可敬。
10 Kumcha Yahwe ni mwanzo wa hekima; wale washikao maagizo yake wana uelewa mzuri. Sifa yake yadumu milele.
敬愛上主,是智慧的開始:實行敬愛的人,算有智慧;他的榮譽,必定存留永世。