< Zaburi 110 >

1 Yahwe humwambia bwana wangu, “Kaa mkono wangu wa kuume mpaka nitakapowaweka adui zako chini ya miguu yako.”
A Psalm of David. The LORD said unto my Lord, Sit thou at my right hand, until I make thine enemies thy footstool.
2 Yahwe atainyosha fimbo ya nguvu yako toka Sayuni; utawale kati ya adui zako.
The LORD shall send the rod of thy strength out of Zion: rule thou in the midst of thine enemies.
3 Siku ile ya uweza wako watu wako watakufuata wakiwa katika mavazi matakatifu ya hiari yao wenyewe; tokea tumbo la alfajiri ujana wako utakuwa kwako kama umande.
Thy people [shall be] willing in the day of thy power, in the beauties of holiness from the womb of the morning: thou hast the dew of thy youth.
4 Yahwe ameapa, na hatabadilika: “Wewe ni kuhani milele, baada ya namna ya Melkizedeki.”
The LORD hath sworn, and will not repent, Thou [art] a priest for ever after the order of Melchizedek.
5 Bwana yuko mkono wako wa kuume. Siku ile ya hasira yake atawaua wafalme.
The Lord at thy right hand shall strike through kings in the day of his wrath.
6 Yeye atahukumu matifa; ataujaza uwanja wa vita kwa maiti; atawauwa viongozi kaitka nchi nyingi.
He shall judge among the heathen, he shall fill [the places] with the dead bodies; he shall wound the heads over many countries.
7 Atakunywa maji ya kijito njiani, kisha baada ya ushindi atainua kichwa chake juu.
He shall drink of the brook in the way: therefore shall he lift up the head.

< Zaburi 110 >