< Zaburi 11 >
1 Ni kwako Yahweh ninapata usalama; ni kwa namna gani utasema na mimi, “Ruka kama ndege hadi mlimani”?
in finem psalmus David in Domino confido quomodo dicitis animae meae transmigra in montes sicut passer
2 Tazama! Waovu wana andaa pinde zao. Wana tayarisha gizani mishale yao kwenye kamba ili kufyatua mioyo ya wenye haki.
quoniam ecce peccatores intenderunt arcum paraverunt sagittas suas in faretra ut sagittent in obscuro rectos corde
3 Ikiwa misingi imeharibiwa, mwenye haki atafanya nini?
quoniam quae perfecisti destruxerunt iustus autem quid fecit
4 Yahweh yuko katika hekalu takatifu; macho yake yanatazama, yakiuchunguza ubinadamu.
Dominus in templo sancto suo Dominus in caelo sedis eius oculi eius in pauperem respiciunt palpebrae eius interrogant filios hominum
5 Yahweh huwachunguza wote wenye haki na waovu, bali huwachukia wapendao kuwaumiza wengine.
Dominus interrogat iustum et impium qui autem diligit iniquitatem odit animam suam
6 Yeye huwanyeshea waovu makaa ya mawe na moto wa jehanamu; upepo uunguzao utakuwa ni sehemu yao kutoka katika kikombe chake!
pluet super peccatores laqueos ignis et sulphur et spiritus procellarum pars calicis eorum
7 Kwa kuwa Yahweh ni mwenye haki, Naye hupenda haki; wenye haki watauona uso wake.
quoniam iustus Dominus et iustitias dilexit aequitatem vidit vultus eius