< Zaburi 109 >
1 Zaburi ya Daudi. Mungu ninaye msifu, usinyamaze kimya.
Al Músico principal: Salmo de David. OH Dios de mi alabanza, no calles;
2 Kwa maana waovu na wadanganyifu wananishambulia; wanazungumza uongo dhidi yangu.
Porque boca de impío y boca de engañador se han abierto sobre mí: han hablado de mí con lengua mentirosa,
3 Wananizunguka na kusema mambo ya chuki, na wananishambulia bila sababu.
Y con palabras de odio me rodearon; y pelearon contra mí sin causa.
4 Wananilipa kashfa badala ya upendo, lakini mimi ninawaombea.
En pago de mi amor me han sido adversarios: mas yo oraba.
5 Wananilipa uovu badala ya mema, na wanachukia upendo wangu.
Y pusieron contra mí mal por bien, y odio por amor.
6 Teua mtu mwovu aliye adui zaidi kama watu hawa; teua mshitaki asimame mkono wake wa kuume.
Pon sobre él al impío: y Satán esté á su diestra.
7 Na atakapohukumiwa, aonekane na hatia; maombi yake yachukuliwe kuwa ni dhambi.
Cuando fuere juzgado, salga impío; y su oración sea para pecado.
8 Siku zake na ziwe chahe; mamlaka yake na yachukuliwe na mtu mwingine.
Sean sus días pocos: tome otro su oficio.
9 Watoto wake wawe yatima, na mke wake awe mjane.
Sean sus hijos huérfanos, y su mujer viuda.
10 Watoto wake wenye kutanga tanga na kuombaomba, wakiondoka katika nyumba zao zilizo haribika na kuomba chakula au pesa kwa wapita njia.
Y anden sus hijos vagabundos, y mendiguen; y procuren [su pan lejos] de sus desolados hogares.
11 Mdai na achukue vitu vyake vyote amilikivyo; wageni wateke mapato ya kazi yake.
Enrede el acreedor todo lo que tiene, y extraños saqueen su trabajo.
12 Asiwepo mtu yeyote wa kumfanyia wema; mtu yeyote asiwahurumie yatima wake.
No tenga quien le haga misericordia; ni haya quien tenga compasión de sus huérfanos.
13 Watoto wake waangamizwe; majina yao na yafutwe katika kizazi kijacho.
Su posteridad sea talada; en segunda generación sea raído su nombre.
14 Uovu wa baba zake utajwe kwa Yahwe; na dhambi ya mama yake isisahaulike.
Venga en memoria cerca de Jehová la maldad de sus padres, y el pecado de su madre no sea borrado.
15 Hatia zao na ziwe mbele ya Yahwe siku zote; Yahwe na aiondoe kumbukumbu yao duniani.
Estén siempre delante de Jehová, y él corte de la tierra su memoria.
16 Yahwe na afanye hivi kwa sababu mtu huyu kamwe hakusumbuka kuonesha uaminifu wa agano wowote, lakini badala yake aliwasumbua wanyonge, wahitaji, na kuwaua walio vunjika moyo.
Por cuanto no se acordó de hacer misericordia, y persiguió al hombre afligido y menesteroso y quebrantado de corazón, para matar[lo].
17 Alipenda kulaani; na imrudie juu yake. Alichukia kubariki; baraka zozote na zisije kwake.
Y amó la maldición, y vínole; y no quiso la bendición, y ella se alejó de él.
18 Alijivika kulaani kana kwamba ni vazi lake, na laana yake iliingia ndani yake kama maji, na kama mafuta mifupani mwake.
Y vistióse de maldición como de su vestido, y entró como agua en sus entrañas, y como aceite en sus huesos.
19 Laana zake na ziwe kwake kama vazi avaalo kujifunika mwenyewe, na kama mkanda avaao kila siku.
Séale como vestido con que se cubra, y en lugar de cinto con que se ciña siempre.
20 Na haya yawe malipo ya mshitaki wangu kutoka kwa Yahwe, ya wale wasemao mambo maovu juu yangu.
Este sea el pago de parte de Jehová de los que me calumnian, y de los que hablan mal contra mi alma.
21 Yahwe Bwana wangu, unishughulikie kwa wema kwa ajili ya jina lako. Kwa sababu uaminifu wa agano lako ni mwema, uniokoe.
Y tú, Jehová Señor, haz conmigo por amor de tu nombre: líbrame, porque tu misericordia es buena.
22 Kwa maana ni mnyonge na muhitaji, na moyo wangu umejeruhiwa ndani yangu.
Porque yo estoy afligido y necesitado; y mi corazón está herido dentro de mí.
23 Ninatoweka kama kivuli cha jioni; ninapeperushwa kama nzige.
Voime como la sombra cuando declina; soy sacudido como langosta.
24 Magoti yangu ni dhaifu kutokana na kufunga; ninakuwa mwembamba na mifupa.
Mis rodillas están debilitadas á causa del ayuno, y mi carne desfallecida por falta de gordura.
25 Nimedharauliwa na washitaki wangu; wanionapo; hutikisa vichwa vyao.
Yo he sido para ellos objeto de oprobio; mirábanme, y meneaban su cabeza.
26 Nisaidie, Yahwe Mungu wangu; uniokoe kwa uaminifu wa agano lako.
Ayúdame, Jehová Dios mío: sálvame conforme á tu misericordia.
27 Nao wajue kuwa wewe umefanya haya, kwamba wewe, Yahwe, umetenda haya.
Y entiendan que esta es tu mano; [que] tú, Jehová, has hecho esto.
28 Ingawa wananilaani, tafadhali unibariki; wanishambuliapo, waaibishwe, lakini mtumishi wako afurahi.
Maldigan ellos, y bendice tú: levántense, mas sean avergonzados, y regocíjese tu siervo.
29 Washitaki wangu na wavishwe kwa aibu; wavae aibu yao kama vazi.
Sean vestidos de ignominia los que me calumnian; y sean cubiertos de su confusión como con manto.
30 Kwa kinywa changu ninatoa shukrani kuu kwa Yahwe; nitamsifu yeye katikati ya kusanyiko.
Yo alabaré á Jehová en gran manera con mi boca, y le loaré en medio de muchos.
31 Maana nitasimama mkono wa kuume wa mhitaji, ili nimuokoe dhidi ya wale wanao muhukumu.
Porque él se pondrá á la diestra del pobre, para librar su alma de los que le juzgan.