< Zaburi 109 >

1 Zaburi ya Daudi. Mungu ninaye msifu, usinyamaze kimya.
In finem. Psalmus David.
2 Kwa maana waovu na wadanganyifu wananishambulia; wanazungumza uongo dhidi yangu.
[Deus, laudem meam ne tacueris, quia os peccatoris et os dolosi super me apertum est.
3 Wananizunguka na kusema mambo ya chuki, na wananishambulia bila sababu.
Locuti sunt adversum me lingua dolosa, et sermonibus odii circumdederunt me: et expugnaverunt me gratis.
4 Wananilipa kashfa badala ya upendo, lakini mimi ninawaombea.
Pro eo ut me diligerent, detrahebant mihi; ego autem orabam.
5 Wananilipa uovu badala ya mema, na wanachukia upendo wangu.
Et posuerunt adversum me mala pro bonis, et odium pro dilectione mea.
6 Teua mtu mwovu aliye adui zaidi kama watu hawa; teua mshitaki asimame mkono wake wa kuume.
Constitue super eum peccatorem, et diabolus stet a dextris ejus.
7 Na atakapohukumiwa, aonekane na hatia; maombi yake yachukuliwe kuwa ni dhambi.
Cum judicatur, exeat condemnatus; et oratio ejus fiat in peccatum.
8 Siku zake na ziwe chahe; mamlaka yake na yachukuliwe na mtu mwingine.
Fiant dies ejus pauci, et episcopatum ejus accipiat alter.
9 Watoto wake wawe yatima, na mke wake awe mjane.
Fiant filii ejus orphani, et uxor ejus vidua.
10 Watoto wake wenye kutanga tanga na kuombaomba, wakiondoka katika nyumba zao zilizo haribika na kuomba chakula au pesa kwa wapita njia.
Nutantes transferantur filii ejus et mendicent, et ejiciantur de habitationibus suis.
11 Mdai na achukue vitu vyake vyote amilikivyo; wageni wateke mapato ya kazi yake.
Scrutetur fœnerator omnem substantiam ejus, et diripiant alieni labores ejus.
12 Asiwepo mtu yeyote wa kumfanyia wema; mtu yeyote asiwahurumie yatima wake.
Non sit illi adjutor, nec sit qui misereatur pupillis ejus.
13 Watoto wake waangamizwe; majina yao na yafutwe katika kizazi kijacho.
Fiant nati ejus in interitum; in generatione una deleatur nomen ejus.
14 Uovu wa baba zake utajwe kwa Yahwe; na dhambi ya mama yake isisahaulike.
In memoriam redeat iniquitas patrum ejus in conspectu Domini, et peccatum matris ejus non deleatur.
15 Hatia zao na ziwe mbele ya Yahwe siku zote; Yahwe na aiondoe kumbukumbu yao duniani.
Fiant contra Dominum semper, et dispereat de terra memoria eorum:
16 Yahwe na afanye hivi kwa sababu mtu huyu kamwe hakusumbuka kuonesha uaminifu wa agano wowote, lakini badala yake aliwasumbua wanyonge, wahitaji, na kuwaua walio vunjika moyo.
pro eo quod non est recordatus facere misericordiam,
17 Alipenda kulaani; na imrudie juu yake. Alichukia kubariki; baraka zozote na zisije kwake.
et persecutus est hominem inopem et mendicum, et compunctum corde, mortificare.
18 Alijivika kulaani kana kwamba ni vazi lake, na laana yake iliingia ndani yake kama maji, na kama mafuta mifupani mwake.
Et dilexit maledictionem, et veniet ei; et noluit benedictionem, et elongabitur ab eo. Et induit maledictionem sicut vestimentum; et intravit sicut aqua in interiora ejus, et sicut oleum in ossibus ejus.
19 Laana zake na ziwe kwake kama vazi avaalo kujifunika mwenyewe, na kama mkanda avaao kila siku.
Fiat ei sicut vestimentum quo operitur, et sicut zona qua semper præcingitur.
20 Na haya yawe malipo ya mshitaki wangu kutoka kwa Yahwe, ya wale wasemao mambo maovu juu yangu.
Hoc opus eorum qui detrahunt mihi apud Dominum, et qui loquuntur mala adversus animam meam.
21 Yahwe Bwana wangu, unishughulikie kwa wema kwa ajili ya jina lako. Kwa sababu uaminifu wa agano lako ni mwema, uniokoe.
Et tu, Domine, Domine, fac mecum propter nomen tuum, quia suavis est misericordia tua.
22 Kwa maana ni mnyonge na muhitaji, na moyo wangu umejeruhiwa ndani yangu.
Libera me, quia egenus et pauper ego sum, et cor meum conturbatum est intra me.
23 Ninatoweka kama kivuli cha jioni; ninapeperushwa kama nzige.
Sicut umbra cum declinat ablatus sum, et excussus sum sicut locustæ.
24 Magoti yangu ni dhaifu kutokana na kufunga; ninakuwa mwembamba na mifupa.
Genua mea infirmata sunt a jejunio, et caro mea immutata est propter oleum.
25 Nimedharauliwa na washitaki wangu; wanionapo; hutikisa vichwa vyao.
Et ego factus sum opprobrium illis; viderunt me, et moverunt capita sua.
26 Nisaidie, Yahwe Mungu wangu; uniokoe kwa uaminifu wa agano lako.
Adjuva me, Domine Deus meus; salvum me fac secundum misericordiam tuam.
27 Nao wajue kuwa wewe umefanya haya, kwamba wewe, Yahwe, umetenda haya.
Et sciant quia manus tua hæc, et tu, Domine, fecisti eam.
28 Ingawa wananilaani, tafadhali unibariki; wanishambuliapo, waaibishwe, lakini mtumishi wako afurahi.
Maledicent illi, et tu benedices: qui insurgunt in me confundantur; servus autem tuus lætabitur.
29 Washitaki wangu na wavishwe kwa aibu; wavae aibu yao kama vazi.
Induantur qui detrahunt mihi pudore, et operiantur sicut diploide confusione sua.
30 Kwa kinywa changu ninatoa shukrani kuu kwa Yahwe; nitamsifu yeye katikati ya kusanyiko.
Confitebor Domino nimis in ore meo, et in medio multorum laudabo eum:
31 Maana nitasimama mkono wa kuume wa mhitaji, ili nimuokoe dhidi ya wale wanao muhukumu.
quia astitit a dextris pauperis, ut salvam faceret a persequentibus animam meam.]

< Zaburi 109 >