< Zaburi 109 >

1 Zaburi ya Daudi. Mungu ninaye msifu, usinyamaze kimya.
聖歌隊の指揮者によってうたわせたダビデの歌 わたしのほめたたえる神よ、もださないでください。
2 Kwa maana waovu na wadanganyifu wananishambulia; wanazungumza uongo dhidi yangu.
彼らは悪しき口と欺きの口をあけて、わたしにむかい、偽りの舌をもってわたしに語り、
3 Wananizunguka na kusema mambo ya chuki, na wananishambulia bila sababu.
恨みの言葉をもってわたしを囲み、ゆえなくわたしを攻めるのです。
4 Wananilipa kashfa badala ya upendo, lakini mimi ninawaombea.
彼らはわが愛にむくいて、わたしを非難します。しかしわたしは彼らのために祈ります。
5 Wananilipa uovu badala ya mema, na wanachukia upendo wangu.
彼らは悪をもってわが善に報い、恨みをもってわが愛に報いるのです。
6 Teua mtu mwovu aliye adui zaidi kama watu hawa; teua mshitaki asimame mkono wake wa kuume.
彼の上に悪しき人を立て、訴える者に彼を訴えさせてください。
7 Na atakapohukumiwa, aonekane na hatia; maombi yake yachukuliwe kuwa ni dhambi.
彼がさばかれるとき、彼を罪ある者とし、その祈を罪に変えてください。
8 Siku zake na ziwe chahe; mamlaka yake na yachukuliwe na mtu mwingine.
その日を少なくし、その財産をほかの人にとらせ、
9 Watoto wake wawe yatima, na mke wake awe mjane.
その子らをみなしごにし、その妻をやもめにしてください。
10 Watoto wake wenye kutanga tanga na kuombaomba, wakiondoka katika nyumba zao zilizo haribika na kuomba chakula au pesa kwa wapita njia.
その子らを放浪者として施しをこわせ、その荒れたすまいから追い出させてください。
11 Mdai na achukue vitu vyake vyote amilikivyo; wageni wateke mapato ya kazi yake.
彼が持っているすべての物を債主に奪わせ、その勤労の実をほかの人にかすめさせてください。
12 Asiwepo mtu yeyote wa kumfanyia wema; mtu yeyote asiwahurumie yatima wake.
彼にいつくしみを施す者はひとりもなく、またそのみなしごをあわれむ者もなく、
13 Watoto wake waangamizwe; majina yao na yafutwe katika kizazi kijacho.
その子孫を絶えさせ、その名を次の代に消し去ってください。
14 Uovu wa baba zake utajwe kwa Yahwe; na dhambi ya mama yake isisahaulike.
その父たちの不義は主のみ前に覚えられ、その母の罪を消し去らないでください。
15 Hatia zao na ziwe mbele ya Yahwe siku zote; Yahwe na aiondoe kumbukumbu yao duniani.
それらを常に主のみ前に置き、彼の記憶を地から断ってください。
16 Yahwe na afanye hivi kwa sababu mtu huyu kamwe hakusumbuka kuonesha uaminifu wa agano wowote, lakini badala yake aliwasumbua wanyonge, wahitaji, na kuwaua walio vunjika moyo.
これは彼がいつくしみを施すことを思わず、かえって貧しい者、乏しい者を責め、心の痛める者を殺そうとしたからです。
17 Alipenda kulaani; na imrudie juu yake. Alichukia kubariki; baraka zozote na zisije kwake.
彼はのろうことを好んだ。のろいを彼に臨ませてください。彼は恵むことを喜ばなかった。恵みを彼から遠ざけてください。
18 Alijivika kulaani kana kwamba ni vazi lake, na laana yake iliingia ndani yake kama maji, na kama mafuta mifupani mwake.
彼はのろいを衣のように着た。のろいを水のようにその身にしみこませ、油のようにその骨にしみこませてください。
19 Laana zake na ziwe kwake kama vazi avaalo kujifunika mwenyewe, na kama mkanda avaao kila siku.
またそれを自分の着る着物のようにならせ、常に締める帯のようにならせてください。
20 Na haya yawe malipo ya mshitaki wangu kutoka kwa Yahwe, ya wale wasemao mambo maovu juu yangu.
これがわたしを非難する者と、わたしに逆らって悪いことを言う者の主からうける報いとしてください。
21 Yahwe Bwana wangu, unishughulikie kwa wema kwa ajili ya jina lako. Kwa sababu uaminifu wa agano lako ni mwema, uniokoe.
しかし、わが主なる神よ、あなたはみ名のために、わたしを顧みてください。あなたのいつくしみの深きにより、わたしをお助けください。
22 Kwa maana ni mnyonge na muhitaji, na moyo wangu umejeruhiwa ndani yangu.
わたしは貧しく、かつ乏しいのです。わたしの心はわがうちに傷ついています。
23 Ninatoweka kama kivuli cha jioni; ninapeperushwa kama nzige.
わたしは夕日の影のように去りゆき、いなごのように追い払われます。
24 Magoti yangu ni dhaifu kutokana na kufunga; ninakuwa mwembamba na mifupa.
わたしのひざは断食によってよろめき、わたしの肉はやせ衰え、
25 Nimedharauliwa na washitaki wangu; wanionapo; hutikisa vichwa vyao.
わたしは彼らにそしられる者となりました。彼らはわたしを見ると、頭を振ります。
26 Nisaidie, Yahwe Mungu wangu; uniokoe kwa uaminifu wa agano lako.
わが神、主よ、わたしをお助けください。あなたのいつくしみにしたがって、わたしをお救いください。
27 Nao wajue kuwa wewe umefanya haya, kwamba wewe, Yahwe, umetenda haya.
主よ、これがあなたのみ手のわざであること、あなたがそれをなされたことを、彼らに知らせてください。
28 Ingawa wananilaani, tafadhali unibariki; wanishambuliapo, waaibishwe, lakini mtumishi wako afurahi.
彼らはのろうけれども、あなたは祝福されます。わたしを攻める者をはずかしめ、あなたのしもべを喜ばせてください。
29 Washitaki wangu na wavishwe kwa aibu; wavae aibu yao kama vazi.
わたしを非難する者にはずかしめを着せ、おのが恥を上着のようにまとわせてください。
30 Kwa kinywa changu ninatoa shukrani kuu kwa Yahwe; nitamsifu yeye katikati ya kusanyiko.
わたしはわが口をもって大いに主に感謝し、多くの人のなかで主をほめたたえます。
31 Maana nitasimama mkono wa kuume wa mhitaji, ili nimuokoe dhidi ya wale wanao muhukumu.
主は貧しい者の右に立って、死罪にさだめようとする者から彼を救われるからです。

< Zaburi 109 >