< Zaburi 109 >
1 Zaburi ya Daudi. Mungu ninaye msifu, usinyamaze kimya.
Psaume de David, [donné] au maître chantre. Ô Dieu de ma louange, ne te tais point.
2 Kwa maana waovu na wadanganyifu wananishambulia; wanazungumza uongo dhidi yangu.
Car la bouche du méchant, et la bouche [remplie] de fraudes se sont ouvertes contre moi, [et] m'ont parlé, en usant d'une langue trompeuse.
3 Wananizunguka na kusema mambo ya chuki, na wananishambulia bila sababu.
Et des paroles pleines de haine m'ont environné, et ils me font la guerre sans cause.
4 Wananilipa kashfa badala ya upendo, lakini mimi ninawaombea.
Au lieu que je les aimais, ils ont été mes ennemis; mais moi, je n'ai fait que prier [en leur faveur].
5 Wananilipa uovu badala ya mema, na wanachukia upendo wangu.
Et ils m'ont rendu le mal pour le bien, et la haine pour l'amour que je leur portais.
6 Teua mtu mwovu aliye adui zaidi kama watu hawa; teua mshitaki asimame mkono wake wa kuume.
Etablis le méchant sur lui, et fais que l'adversaire se tienne à sa droite.
7 Na atakapohukumiwa, aonekane na hatia; maombi yake yachukuliwe kuwa ni dhambi.
Quand il sera jugé, fais qu'il soit déclaré méchant, et que sa prière soit regardée comme un crime.
8 Siku zake na ziwe chahe; mamlaka yake na yachukuliwe na mtu mwingine.
Que sa vie soit courte, et qu'un autre prenne sa charge.
9 Watoto wake wawe yatima, na mke wake awe mjane.
Que ses enfants soient orphelins, et sa femme veuve;
10 Watoto wake wenye kutanga tanga na kuombaomba, wakiondoka katika nyumba zao zilizo haribika na kuomba chakula au pesa kwa wapita njia.
Et que ses enfants soient entièrement vagabonds, et qu'ils mendient et quêtent [en sortant] de leurs maisons détruites.
11 Mdai na achukue vitu vyake vyote amilikivyo; wageni wateke mapato ya kazi yake.
Que le créancier usant d'exaction attrape tout ce qui est à lui, et que les étrangers butinent tout son travail.
12 Asiwepo mtu yeyote wa kumfanyia wema; mtu yeyote asiwahurumie yatima wake.
Qu'il n'y ait personne qui étende sa compassion sur lui, et qu'il n'y ait personne qui ait pitié de ses orphelins.
13 Watoto wake waangamizwe; majina yao na yafutwe katika kizazi kijacho.
Que sa postérité soit exposée à être retranchée; que leur nom soit effacé dans la race qui le suivra.
14 Uovu wa baba zake utajwe kwa Yahwe; na dhambi ya mama yake isisahaulike.
Que l'iniquité de ses pères revienne en mémoire à l'Eternel, et que le péché de sa mère ne soit point effacé.
15 Hatia zao na ziwe mbele ya Yahwe siku zote; Yahwe na aiondoe kumbukumbu yao duniani.
Qu'ils soient continuellement devant l'Eternel; et qu'il retranche leur mémoire de la terre;
16 Yahwe na afanye hivi kwa sababu mtu huyu kamwe hakusumbuka kuonesha uaminifu wa agano wowote, lakini badala yake aliwasumbua wanyonge, wahitaji, na kuwaua walio vunjika moyo.
Parce qu'il ne s'est point souvenu d'user de miséricorde, mais il a persécuté l'homme affligé et misérable, dont le cœur est brisé, et cela pour le faire mourir.
17 Alipenda kulaani; na imrudie juu yake. Alichukia kubariki; baraka zozote na zisije kwake.
Puisqu'il a aimé la malédiction, que la malédiction tombe sur lui; et parce qu'il n'a point pris plaisir à la bénédiction, que la bénédiction aussi s'éloigne de lui.
18 Alijivika kulaani kana kwamba ni vazi lake, na laana yake iliingia ndani yake kama maji, na kama mafuta mifupani mwake.
Et qu'il soit revêtu de malédiction comme de sa robe, et qu'elle entre dans son corps comme de l'eau, et dans ses os comme de l'huile.
19 Laana zake na ziwe kwake kama vazi avaalo kujifunika mwenyewe, na kama mkanda avaao kila siku.
Qu'elle lui soit comme un vêtement dont il se couvre, et comme une ceinture, dont il se ceigne continuellement.
20 Na haya yawe malipo ya mshitaki wangu kutoka kwa Yahwe, ya wale wasemao mambo maovu juu yangu.
Telle soit de part l'Eternel la récompense de mes adversaires, et de ceux qui parlent mal de moi.
21 Yahwe Bwana wangu, unishughulikie kwa wema kwa ajili ya jina lako. Kwa sababu uaminifu wa agano lako ni mwema, uniokoe.
Mais toi, Eternel Seigneur, agis avec moi pour l'amour de ton Nom; [et] parce que ta miséricorde est tendre, délivre-moi.
22 Kwa maana ni mnyonge na muhitaji, na moyo wangu umejeruhiwa ndani yangu.
Car je suis affligé et misérable, et mon cœur est blessé au-dedans de moi.
23 Ninatoweka kama kivuli cha jioni; ninapeperushwa kama nzige.
Je m'en vais comme l'ombre quand elle décline, et je suis chassé comme une sauterelle.
24 Magoti yangu ni dhaifu kutokana na kufunga; ninakuwa mwembamba na mifupa.
Mes genoux sont affaiblis par le jeûne, et ma chair s'est amaigrie, au lieu qu'elle était en bon point.
25 Nimedharauliwa na washitaki wangu; wanionapo; hutikisa vichwa vyao.
Encore leur suis-je en opprobre; quand ils me voient ils branlent la tête.
26 Nisaidie, Yahwe Mungu wangu; uniokoe kwa uaminifu wa agano lako.
Eternel mon Dieu! aide-moi, [et] délivre-moi selon ta miséricorde.
27 Nao wajue kuwa wewe umefanya haya, kwamba wewe, Yahwe, umetenda haya.
Afin qu'on connaisse que c'est ici ta main, et que toi, ô Eternel! tu as fait ceci.
28 Ingawa wananilaani, tafadhali unibariki; wanishambuliapo, waaibishwe, lakini mtumishi wako afurahi.
Ils maudiront, mais tu béniras; ils s'élèveront, mais ils seront confus, et ton serviteur se réjouira.
29 Washitaki wangu na wavishwe kwa aibu; wavae aibu yao kama vazi.
Que mes adversaires soient revêtus de confusion, et couverts de leur honte comme d'un manteau.
30 Kwa kinywa changu ninatoa shukrani kuu kwa Yahwe; nitamsifu yeye katikati ya kusanyiko.
Je célébrerai hautement de ma bouche l'Eternel, et je le louerai au milieu de plusieurs nations.
31 Maana nitasimama mkono wa kuume wa mhitaji, ili nimuokoe dhidi ya wale wanao muhukumu.
De ce qu'il se tient à la droite du misérable, pour le délivrer de ceux qui condamnent son âme.