< Zaburi 109 >
1 Zaburi ya Daudi. Mungu ninaye msifu, usinyamaze kimya.
Au chef des chantres. De David. Psaume. Dieu de ma louange, ne te tais point!
2 Kwa maana waovu na wadanganyifu wananishambulia; wanazungumza uongo dhidi yangu.
Car ils ouvrent contre moi une bouche méchante et trompeuse, Ils me parlent avec une langue mensongère,
3 Wananizunguka na kusema mambo ya chuki, na wananishambulia bila sababu.
Ils m’environnent de discours haineux Et ils me font la guerre sans cause.
4 Wananilipa kashfa badala ya upendo, lakini mimi ninawaombea.
Tandis que je les aime, ils sont mes adversaires; Mais moi je recours à la prière.
5 Wananilipa uovu badala ya mema, na wanachukia upendo wangu.
Ils me rendent le mal pour le bien, Et de la haine pour mon amour.
6 Teua mtu mwovu aliye adui zaidi kama watu hawa; teua mshitaki asimame mkono wake wa kuume.
Place-le sous l’autorité d’un méchant, Et qu’un accusateur se tienne à sa droite!
7 Na atakapohukumiwa, aonekane na hatia; maombi yake yachukuliwe kuwa ni dhambi.
Quand on le jugera, qu’il soit déclaré coupable, Et que sa prière passe pour un péché!
8 Siku zake na ziwe chahe; mamlaka yake na yachukuliwe na mtu mwingine.
Que ses jours soient peu nombreux, Qu’un autre prenne sa charge!
9 Watoto wake wawe yatima, na mke wake awe mjane.
Que ses enfants deviennent orphelins, Et sa femme veuve!
10 Watoto wake wenye kutanga tanga na kuombaomba, wakiondoka katika nyumba zao zilizo haribika na kuomba chakula au pesa kwa wapita njia.
Que ses enfants soient vagabonds et qu’ils mendient, Qu’ils cherchent du pain loin de leur demeure en ruines!
11 Mdai na achukue vitu vyake vyote amilikivyo; wageni wateke mapato ya kazi yake.
Que le créancier s’empare de tout ce qui est à lui, Et que les étrangers pillent le fruit de son travail!
12 Asiwepo mtu yeyote wa kumfanyia wema; mtu yeyote asiwahurumie yatima wake.
Que nul ne conserve pour lui de l’affection, Et que personne n’ait pitié de ses orphelins!
13 Watoto wake waangamizwe; majina yao na yafutwe katika kizazi kijacho.
Que ses descendants soient exterminés, Et que leur nom s’éteigne dans la génération suivante!
14 Uovu wa baba zake utajwe kwa Yahwe; na dhambi ya mama yake isisahaulike.
Que l’iniquité de ses pères reste en souvenir devant l’Éternel, Et que le péché de sa mère ne soit point effacé!
15 Hatia zao na ziwe mbele ya Yahwe siku zote; Yahwe na aiondoe kumbukumbu yao duniani.
Qu’ils soient toujours présents devant l’Éternel, Et qu’il retranche de la terre leur mémoire,
16 Yahwe na afanye hivi kwa sababu mtu huyu kamwe hakusumbuka kuonesha uaminifu wa agano wowote, lakini badala yake aliwasumbua wanyonge, wahitaji, na kuwaua walio vunjika moyo.
Parce qu’il ne s’est pas souvenu d’exercer la miséricorde, Parce qu’il a persécuté le malheureux et l’indigent, Jusqu’à faire mourir l’homme au cœur brisé!
17 Alipenda kulaani; na imrudie juu yake. Alichukia kubariki; baraka zozote na zisije kwake.
Il aimait la malédiction: qu’elle tombe sur lui! Il ne se plaisait pas à la bénédiction: qu’elle s’éloigne de lui!
18 Alijivika kulaani kana kwamba ni vazi lake, na laana yake iliingia ndani yake kama maji, na kama mafuta mifupani mwake.
Qu’il revête la malédiction comme son vêtement, Qu’elle pénètre comme de l’eau dans son intérieur, Comme de l’huile dans ses os!
19 Laana zake na ziwe kwake kama vazi avaalo kujifunika mwenyewe, na kama mkanda avaao kila siku.
Qu’elle lui serve de vêtement pour se couvrir, De ceinture dont il soit toujours ceint!
20 Na haya yawe malipo ya mshitaki wangu kutoka kwa Yahwe, ya wale wasemao mambo maovu juu yangu.
Tel soit, de la part de l’Éternel, le salaire de mes ennemis, Et de ceux qui parlent méchamment de moi!
21 Yahwe Bwana wangu, unishughulikie kwa wema kwa ajili ya jina lako. Kwa sababu uaminifu wa agano lako ni mwema, uniokoe.
Et toi, Éternel, Seigneur! Agis en ma faveur à cause de ton nom, Car ta bonté est grande; délivre-moi!
22 Kwa maana ni mnyonge na muhitaji, na moyo wangu umejeruhiwa ndani yangu.
Je suis malheureux et indigent, Et mon cœur est blessé au-dedans de moi.
23 Ninatoweka kama kivuli cha jioni; ninapeperushwa kama nzige.
Je m’en vais comme l’ombre à son déclin, Je suis chassé comme la sauterelle.
24 Magoti yangu ni dhaifu kutokana na kufunga; ninakuwa mwembamba na mifupa.
Mes genoux sont affaiblis par le jeûne, Et mon corps est épuisé de maigreur.
25 Nimedharauliwa na washitaki wangu; wanionapo; hutikisa vichwa vyao.
Je suis pour eux un objet d’opprobre; Ils me regardent, et secouent la tête.
26 Nisaidie, Yahwe Mungu wangu; uniokoe kwa uaminifu wa agano lako.
Secours-moi, Éternel, mon Dieu! Sauve-moi par ta bonté!
27 Nao wajue kuwa wewe umefanya haya, kwamba wewe, Yahwe, umetenda haya.
Et qu’ils sachent que c’est ta main, Que c’est toi, Éternel, qui l’as fait!
28 Ingawa wananilaani, tafadhali unibariki; wanishambuliapo, waaibishwe, lakini mtumishi wako afurahi.
S’ils maudissent, toi tu béniras; S’ils se lèvent, ils seront confus, Et ton serviteur se réjouira.
29 Washitaki wangu na wavishwe kwa aibu; wavae aibu yao kama vazi.
Que mes adversaires revêtent l’ignominie, Qu’ils se couvrent de leur honte comme d’un manteau!
30 Kwa kinywa changu ninatoa shukrani kuu kwa Yahwe; nitamsifu yeye katikati ya kusanyiko.
Je louerai de ma bouche hautement l’Éternel, Je le célébrerai au milieu de la multitude;
31 Maana nitasimama mkono wa kuume wa mhitaji, ili nimuokoe dhidi ya wale wanao muhukumu.
Car il se tient à la droite du pauvre, Pour le délivrer de ceux qui le condamnent.