< Zaburi 109 >

1 Zaburi ya Daudi. Mungu ninaye msifu, usinyamaze kimya.
Al la ĥorestro. Psalmo de David. Ho Dio, mia gloro, ne silentu.
2 Kwa maana waovu na wadanganyifu wananishambulia; wanazungumza uongo dhidi yangu.
Ĉar buŝon malvirtan kaj buŝon malican ili malfermis kontraŭ mi, Ili parolas kun mi per mensogema lango.
3 Wananizunguka na kusema mambo ya chuki, na wananishambulia bila sababu.
Per vortoj de malamo ili min ĉirkaŭis, Kaj ili militas kontraŭ mi sen mia kulpo.
4 Wananilipa kashfa badala ya upendo, lakini mimi ninawaombea.
Por mia amo ili min malamas; Sed mi preĝas.
5 Wananilipa uovu badala ya mema, na wanachukia upendo wangu.
Ili pagas al mi malbonon por bono Kaj malamon por mia amo.
6 Teua mtu mwovu aliye adui zaidi kama watu hawa; teua mshitaki asimame mkono wake wa kuume.
Metu malvirtulon super lin; Kaj kontraŭulo stariĝu ĉe lia dekstra mano.
7 Na atakapohukumiwa, aonekane na hatia; maombi yake yachukuliwe kuwa ni dhambi.
Kiam li estos juĝata, li eliru kulpa; Kaj lia preĝo estu peko.
8 Siku zake na ziwe chahe; mamlaka yake na yachukuliwe na mtu mwingine.
Liaj tagoj estu malmultaj; Lian oficon ricevu alia.
9 Watoto wake wawe yatima, na mke wake awe mjane.
Liaj infanoj estu orfoj, Kaj lia edzino estu vidvino.
10 Watoto wake wenye kutanga tanga na kuombaomba, wakiondoka katika nyumba zao zilizo haribika na kuomba chakula au pesa kwa wapita njia.
Liaj infanoj vagadu, Kaj ili petu kaj serĉu apud siaj ruinoj.
11 Mdai na achukue vitu vyake vyote amilikivyo; wageni wateke mapato ya kazi yake.
Kreditoro forprenu ĉion, kion li havas; Kaj fremduloj disrabu lian laboron.
12 Asiwepo mtu yeyote wa kumfanyia wema; mtu yeyote asiwahurumie yatima wake.
Neniu faru al li ion bonan; Kaj ne troviĝu kompatanto por liaj orfoj.
13 Watoto wake waangamizwe; majina yao na yafutwe katika kizazi kijacho.
Lia idaro estu kondamnita al ekstermo; En la dua generacio elviŝiĝu ilia nomo.
14 Uovu wa baba zake utajwe kwa Yahwe; na dhambi ya mama yake isisahaulike.
La malbonago de liaj patroj rememoriĝu al la Eternulo, Kaj la peko de lia patrino ne elviŝiĝu.
15 Hatia zao na ziwe mbele ya Yahwe siku zote; Yahwe na aiondoe kumbukumbu yao duniani.
Ili estu ĉiam antaŭ la Eternulo, Kaj Li ekstermu la memoron pri ili de sur la tero.
16 Yahwe na afanye hivi kwa sababu mtu huyu kamwe hakusumbuka kuonesha uaminifu wa agano wowote, lakini badala yake aliwasumbua wanyonge, wahitaji, na kuwaua walio vunjika moyo.
Pro tio, ke li ne memoris fari bonfarojn, Kaj ke li persekutis mizerulon kaj malriĉulon kaj korsuferanton, Por lin mortigi.
17 Alipenda kulaani; na imrudie juu yake. Alichukia kubariki; baraka zozote na zisije kwake.
Li amis malbenon, kaj ĝi venis sur lin; Li ne volis benon, kaj ĝi malproksimiĝis de li.
18 Alijivika kulaani kana kwamba ni vazi lake, na laana yake iliingia ndani yake kama maji, na kama mafuta mifupani mwake.
Li metis sur sin malbenon, kiel veston; Kaj ĝi penetris en lian internon, kiel akvo, Kaj en liajn ostojn, kiel oleo.
19 Laana zake na ziwe kwake kama vazi avaalo kujifunika mwenyewe, na kama mkanda avaao kila siku.
Ĝi estu por li kiel vesto, per kiu li sin kovras, Kaj kiel zono, kiun li ĉiam portas ĉirkaŭ si.
20 Na haya yawe malipo ya mshitaki wangu kutoka kwa Yahwe, ya wale wasemao mambo maovu juu yangu.
Tia estas de la Eternulo la agado kontraŭ miaj kontraŭuloj, Kaj kontraŭ tiuj, kiuj parolas malbonon kontraŭ mia animo.
21 Yahwe Bwana wangu, unishughulikie kwa wema kwa ajili ya jina lako. Kwa sababu uaminifu wa agano lako ni mwema, uniokoe.
Kaj Vi, ho Eternulo, mia Sinjoro, agu kun mi pro Via nomo; Ĉar bona estas Via favorkoreco, savu min.
22 Kwa maana ni mnyonge na muhitaji, na moyo wangu umejeruhiwa ndani yangu.
Ĉar mi estas malriĉulo kaj mizerulo, Kaj mia koro estas rompita en mia interno.
23 Ninatoweka kama kivuli cha jioni; ninapeperushwa kama nzige.
Kiel ombro longiĝanta mi malaperas; Oni forskuas min kiel akridon.
24 Magoti yangu ni dhaifu kutokana na kufunga; ninakuwa mwembamba na mifupa.
Miaj genuoj senfortiĝis de fastado, Kaj mia karno perdis la grason.
25 Nimedharauliwa na washitaki wangu; wanionapo; hutikisa vichwa vyao.
Kaj mi fariĝis mokataĵo por ili; Kiam ili vidas min, ili balancas sian kapon.
26 Nisaidie, Yahwe Mungu wangu; uniokoe kwa uaminifu wa agano lako.
Helpu min, ho Eternulo, mia Dio; Savu min laŭ Via boneco.
27 Nao wajue kuwa wewe umefanya haya, kwamba wewe, Yahwe, umetenda haya.
Kaj oni sciu, ke tio estas Via mano; Ke Vi, ho Eternulo, tion faris.
28 Ingawa wananilaani, tafadhali unibariki; wanishambuliapo, waaibishwe, lakini mtumishi wako afurahi.
Ili malbenas, sed Vi benu; Ili leviĝis, sed ili estos hontigitaj, kaj Via sklavo ĝojos.
29 Washitaki wangu na wavishwe kwa aibu; wavae aibu yao kama vazi.
Miaj kontraŭuloj kovriĝu per malhonoro, Kaj ili envolviĝu en sian honton kiel en veston.
30 Kwa kinywa changu ninatoa shukrani kuu kwa Yahwe; nitamsifu yeye katikati ya kusanyiko.
Mi forte gloros la Eternulon per mia buŝo, Kaj meze de multaj homoj mi Lin laŭdos.
31 Maana nitasimama mkono wa kuume wa mhitaji, ili nimuokoe dhidi ya wale wanao muhukumu.
Ĉar Li staras ĉe la dekstra flanko de malriĉulo, Por savi lin de tiuj, kiuj juĝas lian animon.

< Zaburi 109 >