< Zaburi 109 >
1 Zaburi ya Daudi. Mungu ninaye msifu, usinyamaze kimya.
For the Chief Musician. A Psalm of David. Hold not thy peace, O God of my praise;
2 Kwa maana waovu na wadanganyifu wananishambulia; wanazungumza uongo dhidi yangu.
For the mouth of the wicked and the mouth of deceit have they opened against me: they have spoken unto me with a lying tongue.
3 Wananizunguka na kusema mambo ya chuki, na wananishambulia bila sababu.
They compassed me about also with words of hatred, and fought against me without a cause.
4 Wananilipa kashfa badala ya upendo, lakini mimi ninawaombea.
For my love they are my adversaries: but I [give myself unto] prayer.
5 Wananilipa uovu badala ya mema, na wanachukia upendo wangu.
And they have rewarded me evil for good, and hatred for my love.
6 Teua mtu mwovu aliye adui zaidi kama watu hawa; teua mshitaki asimame mkono wake wa kuume.
Set thou a wicked man over him: and let an adversary stand at his right hand.
7 Na atakapohukumiwa, aonekane na hatia; maombi yake yachukuliwe kuwa ni dhambi.
When he is judged, let him come forth guilty; and let his prayer be turned into sin.
8 Siku zake na ziwe chahe; mamlaka yake na yachukuliwe na mtu mwingine.
Let his days be few; [and] let another take his office.
9 Watoto wake wawe yatima, na mke wake awe mjane.
Let his children be fatherless, and his wife a widow.
10 Watoto wake wenye kutanga tanga na kuombaomba, wakiondoka katika nyumba zao zilizo haribika na kuomba chakula au pesa kwa wapita njia.
Let his children be vagabonds, and beg; and let them seek [their bread] out of their desolate places.
11 Mdai na achukue vitu vyake vyote amilikivyo; wageni wateke mapato ya kazi yake.
Let the extortioner catch all that he hath; and let strangers make spoil of his labour.
12 Asiwepo mtu yeyote wa kumfanyia wema; mtu yeyote asiwahurumie yatima wake.
Let there be none to extend mercy unto him; neither let there be any to have pity on his fatherless children.
13 Watoto wake waangamizwe; majina yao na yafutwe katika kizazi kijacho.
Let his posterity be cut off; in the generation following let their name be blotted out.
14 Uovu wa baba zake utajwe kwa Yahwe; na dhambi ya mama yake isisahaulike.
Let the iniquity of his fathers be remembered with the LORD; and let not the sin of his mother be blotted out.
15 Hatia zao na ziwe mbele ya Yahwe siku zote; Yahwe na aiondoe kumbukumbu yao duniani.
Let them be before the LORD continually, that he may cut off the memory of them from the earth.
16 Yahwe na afanye hivi kwa sababu mtu huyu kamwe hakusumbuka kuonesha uaminifu wa agano wowote, lakini badala yake aliwasumbua wanyonge, wahitaji, na kuwaua walio vunjika moyo.
Because that he remembered not to shew mercy, but persecuted the poor and needy man, and the broken in heart, to slay [them].
17 Alipenda kulaani; na imrudie juu yake. Alichukia kubariki; baraka zozote na zisije kwake.
Yea, he loved cursing, and it came unto him; and he delighted not in blessing, and it was far from him.
18 Alijivika kulaani kana kwamba ni vazi lake, na laana yake iliingia ndani yake kama maji, na kama mafuta mifupani mwake.
He clothed himself also with cursing as with his garment, and it came into his inward parts like water, and like oil into his bones. Let it be unto him as the raiment
19 Laana zake na ziwe kwake kama vazi avaalo kujifunika mwenyewe, na kama mkanda avaao kila siku.
wherewith he covereth himself, and for the girdle wherewith he is girded continually.
20 Na haya yawe malipo ya mshitaki wangu kutoka kwa Yahwe, ya wale wasemao mambo maovu juu yangu.
This is the reward of mine adversaries from the LORD, and of them that speak evil against my soul.
21 Yahwe Bwana wangu, unishughulikie kwa wema kwa ajili ya jina lako. Kwa sababu uaminifu wa agano lako ni mwema, uniokoe.
But deal thou with me, O GOD the Lord, for thy name’s sake: because thy mercy is good, deliver thou me,
22 Kwa maana ni mnyonge na muhitaji, na moyo wangu umejeruhiwa ndani yangu.
For I am poor and needy, and my heart is wounded within me.
23 Ninatoweka kama kivuli cha jioni; ninapeperushwa kama nzige.
I am gone like the shadow when it declineth: I am tossed up and down as the locust.
24 Magoti yangu ni dhaifu kutokana na kufunga; ninakuwa mwembamba na mifupa.
My knees are weak through fasting; and my flesh faileth of fatness.
25 Nimedharauliwa na washitaki wangu; wanionapo; hutikisa vichwa vyao.
I am become also a reproach unto them: when they see me, they shake their head.
26 Nisaidie, Yahwe Mungu wangu; uniokoe kwa uaminifu wa agano lako.
Help me, O LORD my God; O save me according to thy mercy:
27 Nao wajue kuwa wewe umefanya haya, kwamba wewe, Yahwe, umetenda haya.
That they may know that this is thy hand; [that] thou, LORD, hast done it.
28 Ingawa wananilaani, tafadhali unibariki; wanishambuliapo, waaibishwe, lakini mtumishi wako afurahi.
Let them curse, but bless thou: when they arise, they shall be ashamed, but thy servant shall rejoice.
29 Washitaki wangu na wavishwe kwa aibu; wavae aibu yao kama vazi.
Let mine adversaries be clothed with dishonour, and let them cover themselves with their own shame as with a mantle.
30 Kwa kinywa changu ninatoa shukrani kuu kwa Yahwe; nitamsifu yeye katikati ya kusanyiko.
I will give great thanks unto the LORD with my mouth; yea, I will praise him among the multitude.
31 Maana nitasimama mkono wa kuume wa mhitaji, ili nimuokoe dhidi ya wale wanao muhukumu.
For he shall stand at the right hand of the needy, to save him from them that judge his soul.