< Zaburi 109 >
1 Zaburi ya Daudi. Mungu ninaye msifu, usinyamaze kimya.
For the leader. Of David, a psalm. O God whom I praise, keep not silence;
2 Kwa maana waovu na wadanganyifu wananishambulia; wanazungumza uongo dhidi yangu.
for their wicked mouths they have opened against me, they speak to me with tongues that are false,
3 Wananizunguka na kusema mambo ya chuki, na wananishambulia bila sababu.
they beset me with words of hatred, and fight without cause against me.
4 Wananilipa kashfa badala ya upendo, lakini mimi ninawaombea.
My love they requite with hostility, while for them I lift up my prayer.
5 Wananilipa uovu badala ya mema, na wanachukia upendo wangu.
Evil for good they reward me, and hatred for my love.
6 Teua mtu mwovu aliye adui zaidi kama watu hawa; teua mshitaki asimame mkono wake wa kuume.
“Set over him one who is godless,” they say, “an opponent at his right hand.
7 Na atakapohukumiwa, aonekane na hatia; maombi yake yachukuliwe kuwa ni dhambi.
From his trial let him come forth guilty, may his prayer be counted as sin.
8 Siku zake na ziwe chahe; mamlaka yake na yachukuliwe na mtu mwingine.
Grant that his days may be few, that his office be seized by another.
9 Watoto wake wawe yatima, na mke wake awe mjane.
Grant that his children be fatherless, and that his wife be a widow.
10 Watoto wake wenye kutanga tanga na kuombaomba, wakiondoka katika nyumba zao zilizo haribika na kuomba chakula au pesa kwa wapita njia.
Up and down may his children go begging, expelled from their desolate home.
11 Mdai na achukue vitu vyake vyote amilikivyo; wageni wateke mapato ya kazi yake.
May all that he owns be seized by the creditor may strangers plunder the fruits of his toil.
12 Asiwepo mtu yeyote wa kumfanyia wema; mtu yeyote asiwahurumie yatima wake.
“May none extend to him kindness, or pity his fatherless children.
13 Watoto wake waangamizwe; majina yao na yafutwe katika kizazi kijacho.
His descendants be doomed to destruction! Blotted out be his name in one generation!
14 Uovu wa baba zake utajwe kwa Yahwe; na dhambi ya mama yake isisahaulike.
May his father’s guilt be remembered, and his mother’s sin not blotted out:
15 Hatia zao na ziwe mbele ya Yahwe siku zote; Yahwe na aiondoe kumbukumbu yao duniani.
on record always before the Lord, and his memory root from the earth;
16 Yahwe na afanye hivi kwa sababu mtu huyu kamwe hakusumbuka kuonesha uaminifu wa agano wowote, lakini badala yake aliwasumbua wanyonge, wahitaji, na kuwaua walio vunjika moyo.
for he gave no thought to show kindness, but pursued the poor and the needy, drove the downhearted to death.
17 Alipenda kulaani; na imrudie juu yake. Alichukia kubariki; baraka zozote na zisije kwake.
“May the curses he loved light upon him, may the blessings he loathed be afar.
18 Alijivika kulaani kana kwamba ni vazi lake, na laana yake iliingia ndani yake kama maji, na kama mafuta mifupani mwake.
Like a garment he clothed him with curses; may they pierce to his inwards like water, and cling to his bones like oil.
19 Laana zake na ziwe kwake kama vazi avaalo kujifunika mwenyewe, na kama mkanda avaao kila siku.
Let them be like the robe he wraps round him, like the belt he wears every day.”
20 Na haya yawe malipo ya mshitaki wangu kutoka kwa Yahwe, ya wale wasemao mambo maovu juu yangu.
Be this the reward of my adversaries, of those who speak evil against me.
21 Yahwe Bwana wangu, unishughulikie kwa wema kwa ajili ya jina lako. Kwa sababu uaminifu wa agano lako ni mwema, uniokoe.
But you, Lord my God, be true to your name, deal kindly with me; in your gracious kindness save me.
22 Kwa maana ni mnyonge na muhitaji, na moyo wangu umejeruhiwa ndani yangu.
For I am poor and needy, and my heart is wounded within me.
23 Ninatoweka kama kivuli cha jioni; ninapeperushwa kama nzige.
I am gone like a lengthening shadow, I am shaken off like a locust.
24 Magoti yangu ni dhaifu kutokana na kufunga; ninakuwa mwembamba na mifupa.
My knees totter from fasting, my flesh is shrivelled and spare.
25 Nimedharauliwa na washitaki wangu; wanionapo; hutikisa vichwa vyao.
They heap insults upon me: when they see me, they shake their head.
26 Nisaidie, Yahwe Mungu wangu; uniokoe kwa uaminifu wa agano lako.
Help me, O Lord my God, and save me in your kindness.
27 Nao wajue kuwa wewe umefanya haya, kwamba wewe, Yahwe, umetenda haya.
Teach them that this is your hand, and your own doing, O Lord.
28 Ingawa wananilaani, tafadhali unibariki; wanishambuliapo, waaibishwe, lakini mtumishi wako afurahi.
Let them curse, if only you bless. Put my assailants to shame, and make your servant glad.
29 Washitaki wangu na wavishwe kwa aibu; wavae aibu yao kama vazi.
My opponents be clothed with dishonor, and wrapped in a robe of shame.
30 Kwa kinywa changu ninatoa shukrani kuu kwa Yahwe; nitamsifu yeye katikati ya kusanyiko.
I give thanks to you, Lord, with loud voice, I give praise in the midst of the throng;
31 Maana nitasimama mkono wa kuume wa mhitaji, ili nimuokoe dhidi ya wale wanao muhukumu.
for he stands by the poor, at his right hand, to save them from those who condemn them.