< Zaburi 109 >

1 Zaburi ya Daudi. Mungu ninaye msifu, usinyamaze kimya.
For the end, a Psalm of David. For the end, a Psalm of David. O God, pass not over my praise in silence;
2 Kwa maana waovu na wadanganyifu wananishambulia; wanazungumza uongo dhidi yangu.
for the mouth of the sinner and the mouth of the crafty [man] have been opened against me: they have spoken against me with a crafty tongue.
3 Wananizunguka na kusema mambo ya chuki, na wananishambulia bila sababu.
And they have compassed me with words of hatred; and fought against me without a cause.
4 Wananilipa kashfa badala ya upendo, lakini mimi ninawaombea.
Instead of loving me, they falsely accused me: but I continued to pray.
5 Wananilipa uovu badala ya mema, na wanachukia upendo wangu.
And they rewarded me evil for good, and hatred for my love.
6 Teua mtu mwovu aliye adui zaidi kama watu hawa; teua mshitaki asimame mkono wake wa kuume.
Set you a sinner against him; and let the devil stand at his right hand.
7 Na atakapohukumiwa, aonekane na hatia; maombi yake yachukuliwe kuwa ni dhambi.
When he is judged, let him go forth condemned: and let his prayer become sin.
8 Siku zake na ziwe chahe; mamlaka yake na yachukuliwe na mtu mwingine.
Let his days be few: and let another take his office of overseer.
9 Watoto wake wawe yatima, na mke wake awe mjane.
Let his children be orphans, and his wife a widow.
10 Watoto wake wenye kutanga tanga na kuombaomba, wakiondoka katika nyumba zao zilizo haribika na kuomba chakula au pesa kwa wapita njia.
Let his children wander without a dwelling-place, and beg: let them be cast out of their habitations.
11 Mdai na achukue vitu vyake vyote amilikivyo; wageni wateke mapato ya kazi yake.
Let [his] creditor exact all that belongs to him: and let strangers spoil his labours.
12 Asiwepo mtu yeyote wa kumfanyia wema; mtu yeyote asiwahurumie yatima wake.
Let him have no helper; neither let there be any one to have compassion on his fatherless children.
13 Watoto wake waangamizwe; majina yao na yafutwe katika kizazi kijacho.
Let his children be [given up] to utter destruction: in one generation let his name be blotted out.
14 Uovu wa baba zake utajwe kwa Yahwe; na dhambi ya mama yake isisahaulike.
Let the iniquity of his fathers be remembered before the Lord; and let not the sin of his mother be blotted out.
15 Hatia zao na ziwe mbele ya Yahwe siku zote; Yahwe na aiondoe kumbukumbu yao duniani.
Let them be before the Lord continually; and let their memorial be blotted out from the earth.
16 Yahwe na afanye hivi kwa sababu mtu huyu kamwe hakusumbuka kuonesha uaminifu wa agano wowote, lakini badala yake aliwasumbua wanyonge, wahitaji, na kuwaua walio vunjika moyo.
Because he remembered not to show mercy, but persecuted the needy and poor man, and [that] to kill him that was pricked in the heart.
17 Alipenda kulaani; na imrudie juu yake. Alichukia kubariki; baraka zozote na zisije kwake.
He loved cursing also, and it shall come upon him; and he took not pleasure in blessing, so it shall be removed far from him.
18 Alijivika kulaani kana kwamba ni vazi lake, na laana yake iliingia ndani yake kama maji, na kama mafuta mifupani mwake.
Yes, he put on cursing as a garment, and it is come as water into his bowels, and as oil into his bones.
19 Laana zake na ziwe kwake kama vazi avaalo kujifunika mwenyewe, na kama mkanda avaao kila siku.
Let it be to him as a garment which he puts on, and as a girdle with which he girds himself continually.
20 Na haya yawe malipo ya mshitaki wangu kutoka kwa Yahwe, ya wale wasemao mambo maovu juu yangu.
This is the dealing of the Lord with those who falsely accuse me, and of them that speak evil against my soul.
21 Yahwe Bwana wangu, unishughulikie kwa wema kwa ajili ya jina lako. Kwa sababu uaminifu wa agano lako ni mwema, uniokoe.
But you, O Lord, Lord, deal [mercifully] with me, for your name's sake: for your mercy is good.
22 Kwa maana ni mnyonge na muhitaji, na moyo wangu umejeruhiwa ndani yangu.
Deliver me, for I am poor and needy; and my heart is troubled within me.
23 Ninatoweka kama kivuli cha jioni; ninapeperushwa kama nzige.
I am removed as a shadow in its going down: I am tossed up and down like locusts.
24 Magoti yangu ni dhaifu kutokana na kufunga; ninakuwa mwembamba na mifupa.
My knees are weakened through fasting, and my flesh is changed by reason of [the lack of] oil.
25 Nimedharauliwa na washitaki wangu; wanionapo; hutikisa vichwa vyao.
I became also a reproach to them: [when] they saw me they shook their heads.
26 Nisaidie, Yahwe Mungu wangu; uniokoe kwa uaminifu wa agano lako.
Help me, O Lord my God; and save me according to your mercy.
27 Nao wajue kuwa wewe umefanya haya, kwamba wewe, Yahwe, umetenda haya.
And let them know that this is your hand; and [that] you, Lord, have wrought it.
28 Ingawa wananilaani, tafadhali unibariki; wanishambuliapo, waaibishwe, lakini mtumishi wako afurahi.
Let them curse, but you shall bless: let them that rise up against me be ashamed, but let your servant rejoice.
29 Washitaki wangu na wavishwe kwa aibu; wavae aibu yao kama vazi.
Let those that falsely accuse me be clothed with shame, and let them cover themselves with their shame as with a mantle.
30 Kwa kinywa changu ninatoa shukrani kuu kwa Yahwe; nitamsifu yeye katikati ya kusanyiko.
I will give thanks to the Lord abundantly with my mouth; and in the midst of many I will praise him.
31 Maana nitasimama mkono wa kuume wa mhitaji, ili nimuokoe dhidi ya wale wanao muhukumu.
For he stood on the right hand of the poor, to save [me] from them that persecute my soul.

< Zaburi 109 >