< Zaburi 109 >

1 Zaburi ya Daudi. Mungu ninaye msifu, usinyamaze kimya.
For the choirmaster. A Psalm of David. O God of my praise, be not silent.
2 Kwa maana waovu na wadanganyifu wananishambulia; wanazungumza uongo dhidi yangu.
For wicked and deceitful mouths open against me; they speak against me with lying tongues.
3 Wananizunguka na kusema mambo ya chuki, na wananishambulia bila sababu.
They surround me with hateful words and attack me without cause.
4 Wananilipa kashfa badala ya upendo, lakini mimi ninawaombea.
In return for my love they accuse me, but I am a man of prayer.
5 Wananilipa uovu badala ya mema, na wanachukia upendo wangu.
They repay me evil for good, and hatred for my love.
6 Teua mtu mwovu aliye adui zaidi kama watu hawa; teua mshitaki asimame mkono wake wa kuume.
Set over him a wicked man; let an accuser stand at his right hand.
7 Na atakapohukumiwa, aonekane na hatia; maombi yake yachukuliwe kuwa ni dhambi.
When he is tried, let him be found guilty, and may his prayer be regarded as sin.
8 Siku zake na ziwe chahe; mamlaka yake na yachukuliwe na mtu mwingine.
May his days be few; may another take his position.
9 Watoto wake wawe yatima, na mke wake awe mjane.
May his children be fatherless and his wife a widow.
10 Watoto wake wenye kutanga tanga na kuombaomba, wakiondoka katika nyumba zao zilizo haribika na kuomba chakula au pesa kwa wapita njia.
May his children wander as beggars, seeking sustenance far from their ruined homes.
11 Mdai na achukue vitu vyake vyote amilikivyo; wageni wateke mapato ya kazi yake.
May the creditor seize all he owns, and strangers plunder the fruits of his labor.
12 Asiwepo mtu yeyote wa kumfanyia wema; mtu yeyote asiwahurumie yatima wake.
May there be no one to extend kindness to him, and no one to favor his fatherless children.
13 Watoto wake waangamizwe; majina yao na yafutwe katika kizazi kijacho.
May his descendants be cut off; may their name be blotted out from the next generation.
14 Uovu wa baba zake utajwe kwa Yahwe; na dhambi ya mama yake isisahaulike.
May the iniquity of his fathers be remembered before the LORD, and the sin of his mother never be blotted out.
15 Hatia zao na ziwe mbele ya Yahwe siku zote; Yahwe na aiondoe kumbukumbu yao duniani.
May their sins always remain before the LORD, that He may cut off their memory from the earth.
16 Yahwe na afanye hivi kwa sababu mtu huyu kamwe hakusumbuka kuonesha uaminifu wa agano wowote, lakini badala yake aliwasumbua wanyonge, wahitaji, na kuwaua walio vunjika moyo.
For he never thought to show kindness, but pursued the poor and needy and brokenhearted, even to their death.
17 Alipenda kulaani; na imrudie juu yake. Alichukia kubariki; baraka zozote na zisije kwake.
The cursing that he loved, may it fall on him; the blessing in which he refused to delight, may it be far from him.
18 Alijivika kulaani kana kwamba ni vazi lake, na laana yake iliingia ndani yake kama maji, na kama mafuta mifupani mwake.
The cursing that he wore like a coat, may it soak into his body like water, and into his bones like oil.
19 Laana zake na ziwe kwake kama vazi avaalo kujifunika mwenyewe, na kama mkanda avaao kila siku.
May it be like a robe wrapped about him, like a belt tied forever around him.
20 Na haya yawe malipo ya mshitaki wangu kutoka kwa Yahwe, ya wale wasemao mambo maovu juu yangu.
May this be the LORD’s reward to my accusers, to those who speak evil against me.
21 Yahwe Bwana wangu, unishughulikie kwa wema kwa ajili ya jina lako. Kwa sababu uaminifu wa agano lako ni mwema, uniokoe.
But You, O GOD, the Lord, deal kindly with me for the sake of Your name; deliver me by the goodness of Your loving devotion.
22 Kwa maana ni mnyonge na muhitaji, na moyo wangu umejeruhiwa ndani yangu.
For I am poor and needy; my heart is wounded within me.
23 Ninatoweka kama kivuli cha jioni; ninapeperushwa kama nzige.
I am fading away like a lengthening shadow; I am shaken off like a locust.
24 Magoti yangu ni dhaifu kutokana na kufunga; ninakuwa mwembamba na mifupa.
My knees are weak from fasting, and my body grows lean and gaunt.
25 Nimedharauliwa na washitaki wangu; wanionapo; hutikisa vichwa vyao.
I am an object of scorn to my accusers; when they see me, they shake their heads.
26 Nisaidie, Yahwe Mungu wangu; uniokoe kwa uaminifu wa agano lako.
Help me, O LORD my God; save me according to Your loving devotion.
27 Nao wajue kuwa wewe umefanya haya, kwamba wewe, Yahwe, umetenda haya.
Let them know that this is Your hand, that You, O LORD, have done it.
28 Ingawa wananilaani, tafadhali unibariki; wanishambuliapo, waaibishwe, lakini mtumishi wako afurahi.
Though they curse, You will bless. When they rise up, they will be put to shame, but Your servant will rejoice.
29 Washitaki wangu na wavishwe kwa aibu; wavae aibu yao kama vazi.
May my accusers be clothed with disgrace; may they wear their shame like a robe.
30 Kwa kinywa changu ninatoa shukrani kuu kwa Yahwe; nitamsifu yeye katikati ya kusanyiko.
With my mouth I will thank the LORD profusely; I will praise Him in the presence of many.
31 Maana nitasimama mkono wa kuume wa mhitaji, ili nimuokoe dhidi ya wale wanao muhukumu.
For He stands at the right hand of the needy one, to save him from the condemners of his soul.

< Zaburi 109 >