< Zaburi 108 >

1 Ee Mungu, moyo wangu u thabiti; nitaimba, naam, nitaimba sifa pia kwa moyo mkuu.
שיר מזמור לדוד נכון לבי אלהים אשירה ואזמרה אף-כבודי
2 Amka, kinanda na kinubi; nitaamka alfajiri.
עורה הנבל וכנור אעירה שחר
3 Nitakushukuru wewe, Yahwe, kati ya watu; nitakuimbia sifa kati ya mataifa.
אודך בעמים יהוה ואזמרך בלאמים
4 Kwa maana uaminifu wa agano lako ni mkuu juu ya mbingu; na uaminifu wako wafika mawinguni.
כי-גדול מעל-שמים חסדך ועד-שחקים אמתך
5 Ee Mungu, uinuliwe, juu ya mbingu, na utukufu wako utukuke juu ya nchi.
רומה על-שמים אלהים ועל כל-הארץ כבודך
6 Ili kwamba wale uwapendao waokolewe, utuokoe sisi kwa mkono wako wa kuume na unijibu.
למען יחלצון ידידיך הושיעה ימינך וענני
7 Mungu ameongea katika utakatifu wake; “Nitashangilia; nitaigawanya Shekemu na nitalipima bonde la Sukothi.
אלהים דבר בקדשו--אעלזה אחלקה שכם ועמק סכות אמדד
8 Gileadi ni yangu, na manase ni yangu; Ephraimu ni nguvu ya kichwa changu; Yuda ni fimbo yangu ya kifalme.
לי גלעד לי מנשה ואפרים מעוז ראשי יהודה מחקקי
9 Moabu ni bakuli langu la kunawia; nitatupa kiatu changu juu ya Edomu; nitapaza sauti katika ushindi kwa ajili ya Filisti.
מואב סיר רחצי--על-אדום אשליך נעלי עלי-פלשת אתרועע
10 Ni nani atakaye nipeleka kwenye mji imara? Ni nani atakayeniongoza mpaka Edomu?”
מי יבלני עיר מבצר מי נחני עד-אדום
11 Ee Mungu, sio wewe uliyetukataa? Hauendi vitani na jeshi letu.
הלא-אלהים זנחתנו ולא-תצא אלהים בצבאתינו
12 Utupe msaada dhidi ya adui yetu, maana msaada wa wanadamu ni bure.
הבה-לנו עזרת מצר ושוא תשועת אדם
13 Tutashinda kwa msaada wa Mungu; atawakanyaga kwa adui zetu.
באלהים נעשה-חיל והוא יבוס צרינו

< Zaburi 108 >