< Zaburi 108 >

1 Ee Mungu, moyo wangu u thabiti; nitaimba, naam, nitaimba sifa pia kwa moyo mkuu.
Ein Lied. Ein Psalm Davids. Mein Herz ist fest, o Gott; ich will singen und spielen!
2 Amka, kinanda na kinubi; nitaamka alfajiri.
Wache auf, meine Ehre, wache auf, Harfe und Zither; aufwecken will ich die Morgenröte!
3 Nitakushukuru wewe, Yahwe, kati ya watu; nitakuimbia sifa kati ya mataifa.
Ich will dich preisen unter den Völkern, Jahwe, und will dich besingen unter den Nationen!
4 Kwa maana uaminifu wa agano lako ni mkuu juu ya mbingu; na uaminifu wako wafika mawinguni.
Denn groß über den Himmel hinaus ist deine Gnade, und bis zu den Wolken deine Treue.
5 Ee Mungu, uinuliwe, juu ya mbingu, na utukufu wako utukuke juu ya nchi.
Erhebe dich über den Himmel, o Gott, und über die ganze Erde breite sich deine Herrlichkeit.
6 Ili kwamba wale uwapendao waokolewe, utuokoe sisi kwa mkono wako wa kuume na unijibu.
Damit deine Geliebten errettet werden, so hilf nun mit deiner Rechten und erhöre mich!
7 Mungu ameongea katika utakatifu wake; “Nitashangilia; nitaigawanya Shekemu na nitalipima bonde la Sukothi.
Gott hat in seinem Heiligtume geredet: “Ich will frohlocken! “Ich will Sichem verteilen und das Thal Sukkoth ausmessen.
8 Gileadi ni yangu, na manase ni yangu; Ephraimu ni nguvu ya kichwa changu; Yuda ni fimbo yangu ya kifalme.
“Mein ist Gilead, mein ist Manasse, und Ephraim ist die Schutzwehr meines Hauptes, Juda mein Herrscherstab.
9 Moabu ni bakuli langu la kunawia; nitatupa kiatu changu juu ya Edomu; nitapaza sauti katika ushindi kwa ajili ya Filisti.
“Moab ist mein Waschbecken; auf Edom werfe ich meinen Schuh, über Philistäa jauchze ich.”
10 Ni nani atakaye nipeleka kwenye mji imara? Ni nani atakayeniongoza mpaka Edomu?”
Wer führt mich nach der festen Stadt? Wer geleitet mich nach Edom?
11 Ee Mungu, sio wewe uliyetukataa? Hauendi vitani na jeshi letu.
Hast nicht du, o Gott, uns verworfen und ziehst nicht aus, o Gott, mit unseren Heeren?
12 Utupe msaada dhidi ya adui yetu, maana msaada wa wanadamu ni bure.
Schaffe uns Hilfe gegen den Feind, denn eitel ist Menschenhilfe!
13 Tutashinda kwa msaada wa Mungu; atawakanyaga kwa adui zetu.
Mit Gott werden wir Heldenthaten verrichten, und er wird unsere Feinde niedertreten.

< Zaburi 108 >