< Zaburi 108 >

1 Ee Mungu, moyo wangu u thabiti; nitaimba, naam, nitaimba sifa pia kwa moyo mkuu.
A song, a psalm of David. My heart is fixed, God; I will sing, yes, I will sing praises also with my honored heart.
2 Amka, kinanda na kinubi; nitaamka alfajiri.
Wake up, lute and harp; I will wake up the dawn.
3 Nitakushukuru wewe, Yahwe, kati ya watu; nitakuimbia sifa kati ya mataifa.
I will give thanks to you, Yahweh, among the peoples; I will sing praises to you among the nations.
4 Kwa maana uaminifu wa agano lako ni mkuu juu ya mbingu; na uaminifu wako wafika mawinguni.
For your covenant faithfulness is great above the heavens; and your trustworthiness reaches to the skies.
5 Ee Mungu, uinuliwe, juu ya mbingu, na utukufu wako utukuke juu ya nchi.
Be exalted, God, above the heavens, and may your glory be exalted over all the earth.
6 Ili kwamba wale uwapendao waokolewe, utuokoe sisi kwa mkono wako wa kuume na unijibu.
So that those you love may be rescued, rescue us with your right hand and answer me.
7 Mungu ameongea katika utakatifu wake; “Nitashangilia; nitaigawanya Shekemu na nitalipima bonde la Sukothi.
God has spoken in his holiness; “I will rejoice; I will divide Shechem and apportion out the Valley of Succoth.
8 Gileadi ni yangu, na manase ni yangu; Ephraimu ni nguvu ya kichwa changu; Yuda ni fimbo yangu ya kifalme.
Gilead is mine, and Manasseh is mine; Ephraim also is my helmet; Judah is my scepter.
9 Moabu ni bakuli langu la kunawia; nitatupa kiatu changu juu ya Edomu; nitapaza sauti katika ushindi kwa ajili ya Filisti.
Moab is my washbasin; over Edom I will throw my shoe; I will shout in triumph because of Philistia.
10 Ni nani atakaye nipeleka kwenye mji imara? Ni nani atakayeniongoza mpaka Edomu?”
Who will bring me into the strong city? Who will lead me to Edom?”
11 Ee Mungu, sio wewe uliyetukataa? Hauendi vitani na jeshi letu.
God, have you not rejected us? You do not go into battle with our army.
12 Utupe msaada dhidi ya adui yetu, maana msaada wa wanadamu ni bure.
Give us help against the enemy, for man's help is futile.
13 Tutashinda kwa msaada wa Mungu; atawakanyaga kwa adui zetu.
We will triumph with God's help; he will trample down our enemies.

< Zaburi 108 >