< Zaburi 108 >

1 Ee Mungu, moyo wangu u thabiti; nitaimba, naam, nitaimba sifa pia kwa moyo mkuu.
A Song, a Melody: David’s. Fixed, is my heart, O God, I will sing and touch the strings, even mine honour.
2 Amka, kinanda na kinubi; nitaamka alfajiri.
Awake, O harp and lyre, I will awaken the dawn!
3 Nitakushukuru wewe, Yahwe, kati ya watu; nitakuimbia sifa kati ya mataifa.
I will thank thee among the peoples, O Yahweh, and will sing praise unto thee, among the tribes of men.
4 Kwa maana uaminifu wa agano lako ni mkuu juu ya mbingu; na uaminifu wako wafika mawinguni.
For, great, above the heavens, is thy lovingkindness, and, as far as the skies, thy faithfulness.
5 Ee Mungu, uinuliwe, juu ya mbingu, na utukufu wako utukuke juu ya nchi.
Be thou exalted above the heavens, O God, And, above all the earth, be thy glory.
6 Ili kwamba wale uwapendao waokolewe, utuokoe sisi kwa mkono wako wa kuume na unijibu.
To the end thy beloved ones may be delivered, Oh save thou with thy right hand and answer me!
7 Mungu ameongea katika utakatifu wake; “Nitashangilia; nitaigawanya Shekemu na nitalipima bonde la Sukothi.
God, hath spoken in his holiness, I will exult! I will apportion Shechem! And, the Vale of Succoth, will I measure out;
8 Gileadi ni yangu, na manase ni yangu; Ephraimu ni nguvu ya kichwa changu; Yuda ni fimbo yangu ya kifalme.
Mine, is Gilead—mine, Manasseh, but, Ephraim, is the defence of my head, Judah, is my commander’s staff;
9 Moabu ni bakuli langu la kunawia; nitatupa kiatu changu juu ya Edomu; nitapaza sauti katika ushindi kwa ajili ya Filisti.
Moab, is my wash-bowl, Upon Edom, will I throw my shoe, Over Philistia, raise a shout of triumph.
10 Ni nani atakaye nipeleka kwenye mji imara? Ni nani atakayeniongoza mpaka Edomu?”
Who will conduct me to a fortified city? Who will lead me as far as Edom?
11 Ee Mungu, sio wewe uliyetukataa? Hauendi vitani na jeshi letu.
Hast not thou, O God, rejected us? and wilt not go forth, O God, with our hosts.
12 Utupe msaada dhidi ya adui yetu, maana msaada wa wanadamu ni bure.
Grant us help out of distress, for, vain, is the deliverance of man:
13 Tutashinda kwa msaada wa Mungu; atawakanyaga kwa adui zetu.
In God, shall we do valiantly, He himself, therefore, shall tread down our adversaries.

< Zaburi 108 >