< Zaburi 108 >
1 Ee Mungu, moyo wangu u thabiti; nitaimba, naam, nitaimba sifa pia kwa moyo mkuu.
“A psalm of David.” O God! my heart is strengthened! I will sing and give thanks.
2 Amka, kinanda na kinubi; nitaamka alfajiri.
Awake, my soul! awake, my psaltery and harp! I will wake with the early dawn.
3 Nitakushukuru wewe, Yahwe, kati ya watu; nitakuimbia sifa kati ya mataifa.
I will praise thee, O LORD! among the nations; I will sing to thee among the peoples!
4 Kwa maana uaminifu wa agano lako ni mkuu juu ya mbingu; na uaminifu wako wafika mawinguni.
For thy mercy reacheth to the heavens, And thy truth above the clouds.
5 Ee Mungu, uinuliwe, juu ya mbingu, na utukufu wako utukuke juu ya nchi.
Exalt thyself, O God! above the heavens, And thy glory above all the earth!
6 Ili kwamba wale uwapendao waokolewe, utuokoe sisi kwa mkono wako wa kuume na unijibu.
That thy beloved ones may be delivered, Save with thy right hand, and answer me!
7 Mungu ameongea katika utakatifu wake; “Nitashangilia; nitaigawanya Shekemu na nitalipima bonde la Sukothi.
God promiseth in his holiness; I will rejoice; I shall yet divide Shechem, And measure out the valley of Succoth;
8 Gileadi ni yangu, na manase ni yangu; Ephraimu ni nguvu ya kichwa changu; Yuda ni fimbo yangu ya kifalme.
Gilead shall be mine, and mine Manasseh; Ephraim shall be my helmet, And Judah my sceptre.
9 Moabu ni bakuli langu la kunawia; nitatupa kiatu changu juu ya Edomu; nitapaza sauti katika ushindi kwa ajili ya Filisti.
Moab shall be my washbowl; Upon Edom shall I cast my shoe; I shall triumph over Philistia.
10 Ni nani atakaye nipeleka kwenye mji imara? Ni nani atakayeniongoza mpaka Edomu?”
Who will bring me to the strong city? Who will lead me into Edom?
11 Ee Mungu, sio wewe uliyetukataa? Hauendi vitani na jeshi letu.
Wilt not thou, O God! who didst forsake us, Who didst not go forth with our armies?
12 Utupe msaada dhidi ya adui yetu, maana msaada wa wanadamu ni bure.
Give us thine aid in our distress, For vain is the help of man!
13 Tutashinda kwa msaada wa Mungu; atawakanyaga kwa adui zetu.
Through God we shall do valiantly; For he will tread down our enemies.