< Zaburi 108 >

1 Ee Mungu, moyo wangu u thabiti; nitaimba, naam, nitaimba sifa pia kwa moyo mkuu.
“A song or psalm of David.” My heart is firm, O God; I will sing and give praise, even with my spirit.
2 Amka, kinanda na kinubi; nitaamka alfajiri.
Awake, psaltery and harp: I will wake up the morning-dawn.
3 Nitakushukuru wewe, Yahwe, kati ya watu; nitakuimbia sifa kati ya mataifa.
I will give thee thanks among the people, O Lord: and I will sing praises unto thee among the nations.
4 Kwa maana uaminifu wa agano lako ni mkuu juu ya mbingu; na uaminifu wako wafika mawinguni.
For great above the heavens is thy kindness, and thy truth reacheth even unto the skies.
5 Ee Mungu, uinuliwe, juu ya mbingu, na utukufu wako utukuke juu ya nchi.
Exalt thyself above the heavens, O God; and above all the earth thy glory.
6 Ili kwamba wale uwapendao waokolewe, utuokoe sisi kwa mkono wako wa kuume na unijibu.
In order that thy beloved may be delivered: help with thy right hand, and answer me.
7 Mungu ameongea katika utakatifu wake; “Nitashangilia; nitaigawanya Shekemu na nitalipima bonde la Sukothi.
God hath spoken in his holiness: I will exult, I will divide Shechem, and the valley of Succoth will I measure out.
8 Gileadi ni yangu, na manase ni yangu; Ephraimu ni nguvu ya kichwa changu; Yuda ni fimbo yangu ya kifalme.
Mine id Gil'ad, and mine is Menasseh; Ephraim also is the strong-hold of my head; of Judah are my chiefs.
9 Moabu ni bakuli langu la kunawia; nitatupa kiatu changu juu ya Edomu; nitapaza sauti katika ushindi kwa ajili ya Filisti.
Moab is my washpot; upon Edom will I cast my shoe; over Philistia will I triumph.
10 Ni nani atakaye nipeleka kwenye mji imara? Ni nani atakayeniongoza mpaka Edomu?”
Who will bring me into the fortified city? who will lead me as far as Edom?
11 Ee Mungu, sio wewe uliyetukataa? Hauendi vitani na jeshi letu.
Behold, it is thou, O God, who hast cast us off; and thou, O God, goest not forth with our armies.
12 Utupe msaada dhidi ya adui yetu, maana msaada wa wanadamu ni bure.
Give us help against the assailant; for vain is the help of man.
13 Tutashinda kwa msaada wa Mungu; atawakanyaga kwa adui zetu.
Through God shall we do valiantly; for he it is that will tread down our adversaries.

< Zaburi 108 >