< Zaburi 108 >
1 Ee Mungu, moyo wangu u thabiti; nitaimba, naam, nitaimba sifa pia kwa moyo mkuu.
A canticle of a psalm for David himself. My heart is ready, O God, my heart is ready: I will sing, and will give praise, with my glory.
2 Amka, kinanda na kinubi; nitaamka alfajiri.
Arise, my glory; arise, psaltery and harp: I will arise in the morning early.
3 Nitakushukuru wewe, Yahwe, kati ya watu; nitakuimbia sifa kati ya mataifa.
I will praise thee, O Lord, among the people: and I will sing unto thee among the populations.
4 Kwa maana uaminifu wa agano lako ni mkuu juu ya mbingu; na uaminifu wako wafika mawinguni.
For thy mercy is great above the heavens: and thy truth even unto the clouds.
5 Ee Mungu, uinuliwe, juu ya mbingu, na utukufu wako utukuke juu ya nchi.
Be thou exalted, O God, above the heavens, and thy glory over all the earth:
6 Ili kwamba wale uwapendao waokolewe, utuokoe sisi kwa mkono wako wa kuume na unijibu.
That thy beloved may be delivered. Save with thy right hand and hear me.
7 Mungu ameongea katika utakatifu wake; “Nitashangilia; nitaigawanya Shekemu na nitalipima bonde la Sukothi.
God hath spoken in his holiness. I will rejoice, and I will divide Sichem and I will mete out the vale of tabernacles.
8 Gileadi ni yangu, na manase ni yangu; Ephraimu ni nguvu ya kichwa changu; Yuda ni fimbo yangu ya kifalme.
Galaad is mine, and Manasses is mine and Ephraim the protection of my head. Juda is my king:
9 Moabu ni bakuli langu la kunawia; nitatupa kiatu changu juu ya Edomu; nitapaza sauti katika ushindi kwa ajili ya Filisti.
Moab the pot of my hope. Over Edom I will stretch out my shoe: the aliens are become my friends.
10 Ni nani atakaye nipeleka kwenye mji imara? Ni nani atakayeniongoza mpaka Edomu?”
Who will bring me into the strong city? who will lead me into Edom?
11 Ee Mungu, sio wewe uliyetukataa? Hauendi vitani na jeshi letu.
Wilt not thou, O God, who hast cast us off? and wilt not thou, O God, go forth with our armies?
12 Utupe msaada dhidi ya adui yetu, maana msaada wa wanadamu ni bure.
O grant us help from trouble: for vain is the help of man.
13 Tutashinda kwa msaada wa Mungu; atawakanyaga kwa adui zetu.
Through God we shall do mightily: and he will bring our enemies to nothing.