< Zaburi 108 >

1 Ee Mungu, moyo wangu u thabiti; nitaimba, naam, nitaimba sifa pia kwa moyo mkuu.
A song. A Psalm of David. My heart is steadfast, O God; I will sing and make music with all my being.
2 Amka, kinanda na kinubi; nitaamka alfajiri.
Awake, O harp and lyre! I will awaken the dawn.
3 Nitakushukuru wewe, Yahwe, kati ya watu; nitakuimbia sifa kati ya mataifa.
I will praise You, O LORD, among the nations; I will sing Your praises among the peoples.
4 Kwa maana uaminifu wa agano lako ni mkuu juu ya mbingu; na uaminifu wako wafika mawinguni.
For Your loving devotion extends beyond the heavens, and Your faithfulness reaches to the clouds.
5 Ee Mungu, uinuliwe, juu ya mbingu, na utukufu wako utukuke juu ya nchi.
Be exalted, O God, above the heavens; may Your glory cover all the earth.
6 Ili kwamba wale uwapendao waokolewe, utuokoe sisi kwa mkono wako wa kuume na unijibu.
Respond and save us with Your right hand, that Your beloved may be delivered.
7 Mungu ameongea katika utakatifu wake; “Nitashangilia; nitaigawanya Shekemu na nitalipima bonde la Sukothi.
God has spoken from His sanctuary: “I will triumph! I will parcel out Shechem and apportion the Valley of Succoth.
8 Gileadi ni yangu, na manase ni yangu; Ephraimu ni nguvu ya kichwa changu; Yuda ni fimbo yangu ya kifalme.
Gilead is Mine, and Manasseh is Mine; Ephraim is My helmet, Judah is My scepter.
9 Moabu ni bakuli langu la kunawia; nitatupa kiatu changu juu ya Edomu; nitapaza sauti katika ushindi kwa ajili ya Filisti.
Moab is My washbasin; upon Edom I toss My sandal; over Philistia I shout in triumph.”
10 Ni nani atakaye nipeleka kwenye mji imara? Ni nani atakayeniongoza mpaka Edomu?”
Who will bring me to the fortified city? Who will lead me to Edom?
11 Ee Mungu, sio wewe uliyetukataa? Hauendi vitani na jeshi letu.
Have You not rejected us, O God? Will You no longer march out, O God, with our armies?
12 Utupe msaada dhidi ya adui yetu, maana msaada wa wanadamu ni bure.
Give us aid against the enemy, for the help of man is worthless.
13 Tutashinda kwa msaada wa Mungu; atawakanyaga kwa adui zetu.
With God we will perform with valor, and He will trample our enemies.

< Zaburi 108 >