< Zaburi 107 >
1 Mshukuruni Yahwe, maana ni mwema, na uaminifu wa agano lake wadumu milele.
ALABAD á Jehová, porque es bueno; porque para siempre [es] su misericordia.
2 Waseme hivi waliokombolewa na Yahwe, wale aliowaokoa toka mkononi mwa adui.
Dígan[lo] los redimidos de Jehová, los que ha redimido del poder del enemigo,
3 Yeye amewakusanya kutoka nchi za kigeni, kutoka mashariki na magharibi, kutoka kaskazini na kusini.
Y los ha congregado de las tierras, del oriente y del occidente, del aquilón y de la mar.
4 Walitanga-tanga janwani katika njia ya nyika hawakuona mji wa kuishi.
Anduvieron perdidos por el desierto, por la soledad sin camino, no hallando ciudad de población.
5 Kwa sababu walikuwa na njaa na kiu, walikata tamaa kutokana na uchovu.
Hambrientos y sedientos, su alma desfallecía en ellos.
6 Kisha walimuita Yahwe katika shida yao, naye aliwaokoa toka katika dhiki yao.
Habiendo empero clamado á Jehová en su angustia, librólos de sus aflicciones:
7 Aliwaongoza kupitia njia ya moja kwa moja waweze kwenda mjini kuishi humo.
Y dirigiólos por camino derecho, para que viniesen á ciudad de población.
8 Oh ili watu wamsifu Yahwe kwa ajili ya uaminifu wa agano lake na kwa mambo ya ajabu aliowatendea wanadamu!
Alaben la misericordia de Jehová, y sus maravillas para con los hijos de los hombres.
9 Maana hutosheleza shauku za walio na kiu, na hamu ya wale wenye njaa yeye huwashibisha kwa mambo mema.
Porque sació al alma menesterosa, y llenó de bien al alma hambrienta.
10 Baadhi walikaa katika giza na uvuli wa mauti, walifungwa katika mateso na minyororo.
Los que moraban en tinieblas y sombra de muerte, aprisionados en aflicción y en hierros;
11 Hii ni kwa sababu walikuwa wameliasi neno la Mungu na walikataa maelekezo ya Aliye Juu.
Por cuanto fueron rebeldes á las palabras de Jehová, y aborrecieron el consejo del Altísimo,
12 Aliinyenyekesha mioyo yao kupitia magumu; walipata mashaka na hakukuwa na mmoja wa kuwasaidia.
Por lo que quebrantó él con trabajo sus corazones, cayeron y no hubo quien [les] ayudase;
13 Kisha wakamwita Yahwe katika shida yao, naye akawatoa katika dhiki yao.
Luego que clamaron á Jehová en su angustia, librólos de sus aflicciones.
14 Aliwatoa gizani na kwenye uvuli wa mauti na kuvunja vifungo vyao.
Sacólos de las tinieblas y de la sombra de muerte, y rompió sus prisiones.
15 Oh ili watu wamsifu Yahwe kwa ajili ya uaminifu wa agano lake na kwa mambo ya ajabu aliyoyatenda kwa wanadamu!
Alaben la misericordia de Jehová, y sus maravillas para con los hijos de los hombres.
16 Kwa maana amevunja malango ya shaba na kukata mapingo ya chuma.
Porque quebrantó las puertas de bronce, y desmenuzó los cerrojos de hierro.
17 Walikuwa wapumbavu katika njia zao za uasi na kuteswa kwa sababu ya dhambi zao.
Los insensatos, á causa del camino de su rebelión y á causa de sus maldades, fueron afligidos.
18 Walipoteza hamu yao ya kula chakula chochote, na waliyakaribia malango ya kifo.
Su alma abominó toda vianda, y llegaron hasta las puertas de la muerte.
19 Kisha walimlilia Yahwe katika shida yao, naye akawatoa katika dhiki yao.
Mas clamaron á Jehová en su angustia, y salvólos de sus aflicciones.
20 Alituma neno lake na likawaponya, na akawaokoa kutoka katika uharibifu wao.
Envió su palabra, y curólos, y librólos de su ruina.
21 Oh ili watu wamsifu Yahwe kwa ajili ya uaminifu wa agano lake na kwa mambo ya ajabu aliyoyatenda kwa wanadamu!
Alaben la misericordia de Jehová, y sus maravillas para con los hijos de los hombres:
22 Na watoe dhabihu ya shukrani na kutangaza matendo yake kwa kuimba.
Y sacrifiquen sacrificios de alabanza, y publiquen sus obras con júbilo.
23 Baadhi husafiri baharini katika meli na kufanya biashara juu ya bahari.
Los que descienden á la mar en navíos, y hacen negocio en las muchas aguas,
24 Hawa huona matendo ya Yahwe na maajabu yake baharini.
Ellos han visto las obras de Jehová, y sus maravillas en el profundo.
25 Kwa maana aliamuru na alivumisha upepo wa dhoruba ambao uliyainua juu mawimbi ya baharini.
El dijo, é hizo saltar el viento de la tempestad, que levanta sus ondas.
26 Walipanda juu mawinguni na kushuka vilindini. Nafsi zao ziliyeyuka katika dhiki.
Suben á los cielos, descienden á los abismos: sus almas se derriten con el mal.
27 Waliyumba-yumba na kupepesuka kama walevi na hawakujua la kufanya.
Tiemblan, y titubean como borrachos, y toda su ciencia es perdida.
28 Kisha walimlilia Yahwe katika shida yao, naye akawatoa katika dhiki yao.
Claman empero á Jehová en su angustia, y líbralos de sus aflicciones.
29 Aliituliza dhoruba, na mawimbi yakatulia.
Hace parar la tempestad en sosiego, y se apaciguan sus ondas.
30 Ndipo walifurahia kwa sababu bahari ilikuwa shwali, na aliwaleta kwenye bandari waliyoitamani.
Alégranse luego porque se reposaron; y él los guía al puerto que deseaban.
31 Oh, ili watu wamsifu Yahwe kwa ajili ya uaminifu wa agano lake na kwa mambo ya ajabu aliyowatendea wanadamu!
Alaben la misericordia de Jehová, y sus maravillas para con los hijos de los hombres.
32 Wamtukuze yeye katika kusanyiko la watu na wamsifu yeye katika baraza la viongozi.
Y ensálcenlo en la congregación del pueblo; y en consistorio de ancianos lo alaben.
33 Aligeuza mito ikwa jangwa, chemchem ya maji ikawa nchi kame,
El vuelve los ríos en desierto, y los manantiales de las aguas en secadales;
34 na nchi ya matunda mengi ikawa nchi isiyozaa kwa sababu ya uovu wa watu wake.
La tierra fructífera en salados, por la maldad de los que la habitan.
35 Aligeuza jangwa likawa ziwa la maji na nchi kame ikawa chemchem ya maji.
Vuelve el desierto en estanques de aguas, y la tierra seca en manantiales.
36 Aliwakalisha huko wenye njaa, nao walijenga mji na kuishi humo.
Y allí aposenta á los hambrientos, y disponen ciudad para habitación;
37 Walijenga mji ili kupanda mimea shambani, kupanda mizabibu, na kuleta humo mazao tele.
Y siembran campos, y plantan viñas, y rinden crecido fruto.
38 Yeye huwabariki wameongezeka sana katika hesabu. Haachi mifugo yao ipungue katika hesabu.
Y los bendice, y se multiplican en gran manera; y no disminuye sus bestias.
39 Kisha wakapungua na kudhilika kwa dhiki na mateso.
Y luego son menoscabados y abatidos á causa de tiranía, de males y congojas.
40 Akawamwagia viongozi dharau na akawafanya wazunguke katika jangwa, mahali pasipo na njia.
El derrama menosprecio sobre los príncipes, y les hace andar errados, vagabundos, sin camino:
41 Lakini aliwalinda wahitaji dhidi ya mateso na kujali kwa ajili ya familia yake kama kundi la kondoo.
Y levanta al pobre de la miseria, y hace [multiplicar] las familias como [rebaños de] ovejas.
42 Wenye haki wataona hili na kufurahi, na uovu wote utaona na kufunga kinya chake.
Vean los rectos, y alégrense; y toda maldad cierre su boca.
43 Yeyote mwenye hekima anapaswa kuyaangalia haya na kutafakari juu ya matendo ya uaminifu wa agano la Yahwe.
¿Quién es sabio y guardará estas cosas, y entenderá las misericordias de Jehová?