< Zaburi 107 >

1 Mshukuruni Yahwe, maana ni mwema, na uaminifu wa agano lake wadumu milele.
Andriañeñe t’Iehovà, amy te Ie ro soa; nainai’e ty fiferenaiña’e.
2 Waseme hivi waliokombolewa na Yahwe, wale aliowaokoa toka mkononi mwa adui.
Ano izay ry jineba’ Iehovà— ry nijebañe’e am-pitàn-drafelahy,
3 Yeye amewakusanya kutoka nchi za kigeni, kutoka mashariki na magharibi, kutoka kaskazini na kusini.
vaho hinoloholo’e hirik’ amo taneo, boak’atiñanañe naho ­ahandrefañ’ añe, boak’ avaratse vaho hirik’ amy riakey.
4 Walitanga-tanga janwani katika njia ya nyika hawakuona mji wa kuishi.
Nirererere ambabangoañ’ añe iereo, an-dratraratra ao, tsy nahaonin-drova fimoneñañe.
5 Kwa sababu walikuwa na njaa na kiu, walikata tamaa kutokana na uchovu.
Nisalikoeñe naho taliñiereñe, nitoirañe añ’ova ao ty fiai’ iareo.
6 Kisha walimuita Yahwe katika shida yao, naye aliwaokoa toka katika dhiki yao.
Le nitoreo am’ Iehovà an-kaloviloviañe naho hinaha’e amo hasotria’iareoo,
7 Aliwaongoza kupitia njia ya moja kwa moja waweze kwenda mjini kuishi humo.
Nindese’e mb’an-dalam-bantam-beo higodañe mb’an-drova fimoneñañe añe.
8 Oh ili watu wamsifu Yahwe kwa ajili ya uaminifu wa agano lake na kwa mambo ya ajabu aliowatendea wanadamu!
Handriañe’ iereo t’Iehovà ty amy fiferenaiña’ey naho o fitoloña’e fanjaka amo ana’ondatioo,
9 Maana hutosheleza shauku za walio na kiu, na hamu ya wale wenye njaa yeye huwashibisha kwa mambo mema.
fa nieneñe’e ty fiaiñe taliñiereñe, nanjañe’e raha soa ty troke nilimpoa.
10 Baadhi walikaa katika giza na uvuli wa mauti, walifungwa katika mateso na minyororo.
Teo ty nitozòke añ’ieñe ao naho an-talinjon-kavilasy ao, rinohy an-kasotriañe naho vý,
11 Hii ni kwa sababu walikuwa wameliasi neno la Mungu na walikataa maelekezo ya Aliye Juu.
amy t’ie niody amo fepèn’Añahareo, vaho nañovok’ i famerea’ i Andindimoneñey.
12 Aliinyenyekesha mioyo yao kupitia magumu; walipata mashaka na hakukuwa na mmoja wa kuwasaidia.
Aa le nampibokohe’e ty arofo’ iareo am-pitromahañe, nampidaleandaleañe tsy amam-pañimba.
13 Kisha wakamwita Yahwe katika shida yao, naye akawatoa katika dhiki yao.
Le nitoreo am’ Iehovà t’ie niankoheke, le rinomba’e amo fikoretañeo;
14 Aliwatoa gizani na kwenye uvuli wa mauti na kuvunja vifungo vyao.
naaka’e boak’ añ’ieñe naho an-talinjon-kavilasy ao, vaho nipoñafe’e o silisilio.
15 Oh ili watu wamsifu Yahwe kwa ajili ya uaminifu wa agano lake na kwa mambo ya ajabu aliyoyatenda kwa wanadamu!
Handriañe’ iareo t’i Iehovà ty amy fiferenaiña’ey naho o halatsañe nanoe’e amo ana’ ondatioo,
16 Kwa maana amevunja malango ya shaba na kukata mapingo ya chuma.
amy te pinaratsà’e o lalam-bey torisìkeo naho pinozapoza’e o doda viñeo.
17 Walikuwa wapumbavu katika njia zao za uasi na kuteswa kwa sababu ya dhambi zao.
Nampisotriañe o seretseo ty amo fiolà’eo, naho o tahi’eo.
18 Walipoteza hamu yao ya kula chakula chochote, na waliyakaribia malango ya kifo.
Nampangori’ ty fiai’ iareo ze atao hàneñe, ie nitotoke o lalam-bein-kavilasio.
19 Kisha walimlilia Yahwe katika shida yao, naye akawatoa katika dhiki yao.
Le nitoreo am’ Iehovà t’ie niampoheke, vaho rinomba’e amo haemberañeo.
20 Alituma neno lake na likawaponya, na akawaokoa kutoka katika uharibifu wao.
Nahitri’e i tsara’ey nahajangañe iareo vaho navotso’e amy kiboriy.
21 Oh ili watu wamsifu Yahwe kwa ajili ya uaminifu wa agano lake na kwa mambo ya ajabu aliyoyatenda kwa wanadamu!
Andriañe’ iereo t’Iehovà ty amy fiferenaiña’ey naho o halatsañe fanoe’e amo ana’ondatioo,
22 Na watoe dhabihu ya shukrani na kutangaza matendo yake kwa kuimba.
Ee t’ie hibanabana sorom- pañandriañañe naho hitalily o fitoloña’eo an-drebeke;
23 Baadhi husafiri baharini katika meli na kufanya biashara juu ya bahari.
Ao ty mizotso mb’an-tsambo an-driake ey; o mpanao balibalik’ an-drano mieneneo,
24 Hawa huona matendo ya Yahwe na maajabu yake baharini.
Fa niisa’ iareo o sata’ Iehovào, o halatsàñe fanoe’e an-dalekeo.
25 Kwa maana aliamuru na alivumisha upepo wa dhoruba ambao uliyainua juu mawimbi ya baharini.
Amy tsara’ey, nitroatse ty tio-bey, nampitoabotse o alon-driakeo.
26 Walipanda juu mawinguni na kushuka vilindini. Nafsi zao ziliyeyuka katika dhiki.
Nionjomb’an-dindimb’eo iereo, vaho nizotso mb’an-dalek’ ao; nitranak’ ami’ty hekoheko’e ty fiai’iareo.
27 Waliyumba-yumba na kupepesuka kama walevi na hawakujua la kufanya.
Nivembeñe, nisiotsiotse hoe jike; fonga nilesa ty hihi’ iareo.
28 Kisha walimlilia Yahwe katika shida yao, naye akawatoa katika dhiki yao.
Nitoreove’ iareo t’Iehovà an-kasosorañe, vaho natsoa’e an-kasotriañe.
29 Aliituliza dhoruba, na mawimbi yakatulia.
Nampipendreñe’e i tio-beiy, le nitsiñe o onjan-driakeo.
30 Ndipo walifurahia kwa sababu bahari ilikuwa shwali, na aliwaleta kwenye bandari waliyoitamani.
Niehake iereo te nibànatse, vaho nitehafe’e mb’amy fipalirañe nisalalaeñey.
31 Oh, ili watu wamsifu Yahwe kwa ajili ya uaminifu wa agano lake na kwa mambo ya ajabu aliyowatendea wanadamu!
Handriañe’ iereo t’Iehovà ty amy fiferenaiña’ey, naho o halatsañe fanoe’e amo ana’ ondatioo.
32 Wamtukuze yeye katika kusanyiko la watu na wamsifu yeye katika baraza la viongozi.
Ee t’ie honjone’ iareo am-pivori’ ondatio vaho handrenge Aze ami’ty fiambesa’ o androanavio.
33 Aligeuza mito ikwa jangwa, chemchem ya maji ikawa nchi kame,
Afote’e ho ratraratra o sakao, naho ho tane kankañe o torahañeo;
34 na nchi ya matunda mengi ikawa nchi isiyozaa kwa sababu ya uovu wa watu wake.
ho fatran-tsira ty tane kobokara, ty ami’ty tsihavokara’ o mpitobok’ ama’eo.
35 Aligeuza jangwa likawa ziwa la maji na nchi kame ikawa chemchem ya maji.
Ampanginakinahe’e o tane mihedatseo, vaho ampanganahanae’e o kirikintañeo;
36 Aliwakalisha huko wenye njaa, nao walijenga mji na kuishi humo.
hampitobea’e o limpoañeo, hañoreña’iareo rova fimoneñañe.
37 Walijenga mji ili kupanda mimea shambani, kupanda mizabibu, na kuleta humo mazao tele.
Handrarake an-teteke ao iereo, naho hambole tetem-bahe, vaho hanonton-tsabo vokatse;
38 Yeye huwabariki wameongezeka sana katika hesabu. Haachi mifugo yao ipungue katika hesabu.
Tahie’e ka iereo hanaranàha’e maro, le tsy apo’e hiha-rìtse o añombe’eo.
39 Kisha wakapungua na kudhilika kwa dhiki na mateso.
Ie nitaketrake iereo, ninìke ami’ty famorekekeañe, naho fanilofañe, vaho anahelo;
40 Akawamwagia viongozi dharau na akawafanya wazunguke katika jangwa, mahali pasipo na njia.
ampidoaña’e ìnje o roandriañeo, ampiriorioe’e am-bangý tsy aman-dalañe añe,
41 Lakini aliwalinda wahitaji dhidi ya mateso na kujali kwa ajili ya familia yake kama kundi la kondoo.
toe aonjo’e ambone’ o hasotriañeo i rarakey, vaho anoe hoe lia-raike o hasavereña’eo.
42 Wenye haki wataona hili na kufurahi, na uovu wote utaona na kufunga kinya chake.
Isa’ o vantañeo izay le mifale, fonga mamìm-bava ka ty hatsivokarañe.
43 Yeyote mwenye hekima anapaswa kuyaangalia haya na kutafakari juu ya matendo ya uaminifu wa agano la Yahwe.
Ia ty mahihitse, hiharaharà’e? ie ro mahafohiñe ty fiferenaiña’ Iehovà.

< Zaburi 107 >