< Zaburi 107 >

1 Mshukuruni Yahwe, maana ni mwema, na uaminifu wa agano lake wadumu milele.
Bekennet Jehovah; denn Er ist gut, denn Seine Barmherzigkeit ist ewig,
2 Waseme hivi waliokombolewa na Yahwe, wale aliowaokoa toka mkononi mwa adui.
Sprechen die Erlösten Jehovahs, die Er aus des Drängers Hand erlöst hat,
3 Yeye amewakusanya kutoka nchi za kigeni, kutoka mashariki na magharibi, kutoka kaskazini na kusini.
Und sie zusammen hat gebracht aus den Ländern vom Aufgang und vom Abend, von Mitternacht und vom Meere.
4 Walitanga-tanga janwani katika njia ya nyika hawakuona mji wa kuishi.
Sie irrten in der Wüste, im Wüstenland, des Weges, sie fanden keine Stadt, um darinnen zu wohnen;
5 Kwa sababu walikuwa na njaa na kiu, walikata tamaa kutokana na uchovu.
Hungernd, auch dürstend, ihre Seele verzagte in ihnen.
6 Kisha walimuita Yahwe katika shida yao, naye aliwaokoa toka katika dhiki yao.
Und sie schrien zu Jehovah in ihrer Drangsal, aus ihren Ängsten rettete Er sie.
7 Aliwaongoza kupitia njia ya moja kwa moja waweze kwenda mjini kuishi humo.
Und ließ sie den geraden Weg gehen, daß sie zur Stadt gingen, um darinnen zu wohnen.
8 Oh ili watu wamsifu Yahwe kwa ajili ya uaminifu wa agano lake na kwa mambo ya ajabu aliowatendea wanadamu!
Sie sollen Jehovah bekennen ob Seiner Barmherzigkeit, und ob Seiner Wunder an den Söhnen des Menschen.
9 Maana hutosheleza shauku za walio na kiu, na hamu ya wale wenye njaa yeye huwashibisha kwa mambo mema.
Daß Er sättigt die lechzende Seele, und die hungernde Seele mit Gutem erfüllt.
10 Baadhi walikaa katika giza na uvuli wa mauti, walifungwa katika mateso na minyororo.
Die, so in Finsternis und Todesschatten saßen, im Elend und in Eisen gebunden,
11 Hii ni kwa sababu walikuwa wameliasi neno la Mungu na walikataa maelekezo ya Aliye Juu.
Weil Gottes Reden sie sich widersetzt, und den Rat des Höchsten gelästert hatten,
12 Aliinyenyekesha mioyo yao kupitia magumu; walipata mashaka na hakukuwa na mmoja wa kuwasaidia.
Und Er beugte ihr Herz durch Mühsal. Sie strauchelten, und niemand stand ihnen bei.
13 Kisha wakamwita Yahwe katika shida yao, naye akawatoa katika dhiki yao.
Und sie schrien zu Jehovah in ihrer Drangsal, und Er rettete sie aus ihren Ängsten,
14 Aliwatoa gizani na kwenye uvuli wa mauti na kuvunja vifungo vyao.
Und brachte sie heraus aus Finsternis und Todesschatten, und riß ab ihre Bande.
15 Oh ili watu wamsifu Yahwe kwa ajili ya uaminifu wa agano lake na kwa mambo ya ajabu aliyoyatenda kwa wanadamu!
Sie sollen Jehovah bekennen ob Seiner Barmherzigkeit, und ob Seiner Wunder an den Söhnen des Menschen.
16 Kwa maana amevunja malango ya shaba na kukata mapingo ya chuma.
Daß Er eherne Türen brach und eiserne Riegel zerhieb.
17 Walikuwa wapumbavu katika njia zao za uasi na kuteswa kwa sababu ya dhambi zao.
Die Törichten, ob dem Wege ihrer Übertretung und ob ihren Missetaten wurden sie gedemütigt.
18 Walipoteza hamu yao ya kula chakula chochote, na waliyakaribia malango ya kifo.
Daß ihrer Seele vor aller Speise graute, und sie die Tore des Todes berührten.
19 Kisha walimlilia Yahwe katika shida yao, naye akawatoa katika dhiki yao.
Und sie schrien zu Jehovah in ihrer Drangsal, aus ihren Ängsten rettete Er sie.
20 Alituma neno lake na likawaponya, na akawaokoa kutoka katika uharibifu wao.
Er sandte Sein Wort und heilte sie, und ließ sie entrinnen aus ihren Gruben.
21 Oh ili watu wamsifu Yahwe kwa ajili ya uaminifu wa agano lake na kwa mambo ya ajabu aliyoyatenda kwa wanadamu!
Sie sollen Jehovah bekennen ob Seiner Barmherzigkeit und ob Seiner Wunder an den Söhnen des Menschen.
22 Na watoe dhabihu ya shukrani na kutangaza matendo yake kwa kuimba.
Und sie sollen Opfer des Dankes opfern, und erzählen Seine Taten mit Lobpreisung.
23 Baadhi husafiri baharini katika meli na kufanya biashara juu ya bahari.
Die hinabsteigen auf das Meer in Schiffen, die Geschäft tun auf vielen Wassern;
24 Hawa huona matendo ya Yahwe na maajabu yake baharini.
Sie sehen Jehovahs Taten, und Seine Wunder in dem Schlunde.
25 Kwa maana aliamuru na alivumisha upepo wa dhoruba ambao uliyainua juu mawimbi ya baharini.
Er spricht und läßt erstehen des Sturmes Wind, der seine Wogen emporhebt;
26 Walipanda juu mawinguni na kushuka vilindini. Nafsi zao ziliyeyuka katika dhiki.
Sie steigen hinauf zum Himmel, sie fahren hinab in Abgründe, ihre Seele zerfließt vor Bösem.
27 Waliyumba-yumba na kupepesuka kama walevi na hawakujua la kufanya.
Sie taumeln und schwanken wie ein Trunkener, und all ihre Weisheit ist verschlungen.
28 Kisha walimlilia Yahwe katika shida yao, naye akawatoa katika dhiki yao.
Und sie schreien zu Jehovah in ihrer Drangsal, und aus ihren Ängsten bringt Er sie heraus.
29 Aliituliza dhoruba, na mawimbi yakatulia.
Er läßt zur Stille erstehen den Sturm, und ihre Wogen schweigen.
30 Ndipo walifurahia kwa sababu bahari ilikuwa shwali, na aliwaleta kwenye bandari waliyoitamani.
Und sie sind fröhlich, daß sie zur Ruhe kommen, und Er führt sie zum Hafen ihrer Lust.
31 Oh, ili watu wamsifu Yahwe kwa ajili ya uaminifu wa agano lake na kwa mambo ya ajabu aliyowatendea wanadamu!
Sie sollen Jehovah bekennen ob Seiner Barmherzigkeit und ob Seiner Wunder an des Menschen Söhnen.
32 Wamtukuze yeye katika kusanyiko la watu na wamsifu yeye katika baraza la viongozi.
Und sie sollen Ihn erhöhen in der Versammlung des Volkes, und Ihn loben auf dem Sitze der Alten.
33 Aligeuza mito ikwa jangwa, chemchem ya maji ikawa nchi kame,
Flüsse setzt Er zur Wüste, die Ausflüsse des Wassers zum Durstland.
34 na nchi ya matunda mengi ikawa nchi isiyozaa kwa sababu ya uovu wa watu wake.
Ein fruchtbar Land zum Salzgrund, ob der Bosheit derer, die darin wohnen.
35 Aligeuza jangwa likawa ziwa la maji na nchi kame ikawa chemchem ya maji.
Die Wüste setzt Er zum Teich der Wasser, und dürres Land zu Ausflüssen der Wasser.
36 Aliwakalisha huko wenye njaa, nao walijenga mji na kuishi humo.
Und läßt Hungrige dort wohnen, daß eine Stadt sie bereiten zum Wohnen.
37 Walijenga mji ili kupanda mimea shambani, kupanda mizabibu, na kuleta humo mazao tele.
Und daß Felder sie besäen, und Weinberge pflanzen und machen des Ertrages Frucht.
38 Yeye huwabariki wameongezeka sana katika hesabu. Haachi mifugo yao ipungue katika hesabu.
Und Er segnet sie, daß sie sich sehr mehren, und macht ihres Viehs nicht wenig.
39 Kisha wakapungua na kudhilika kwa dhiki na mateso.
Und ihrer waren wenig und sie beugten sich ob des Zwanges von Übel und Gram.
40 Akawamwagia viongozi dharau na akawafanya wazunguke katika jangwa, mahali pasipo na njia.
Er goß Verachtung auf die Edlen und ließ sie irren in der Öde ohne Weg.
41 Lakini aliwalinda wahitaji dhidi ya mateso na kujali kwa ajili ya familia yake kama kundi la kondoo.
Und Er hebt in die Höhe aus dem Elend den Dürftigen und setzt die Familien wie eine Herde.
42 Wenye haki wataona hili na kufurahi, na uovu wote utaona na kufunga kinya chake.
Die Redlichen sehen es und sind fröhlich, und aller Verkehrtheit wird ihr Mund zugestopft.
43 Yeyote mwenye hekima anapaswa kuyaangalia haya na kutafakari juu ya matendo ya uaminifu wa agano la Yahwe.
Wer ist weise und behält dies, und versteht Jehovahs Barmherzigkeit?

< Zaburi 107 >