< Zaburi 107 >
1 Mshukuruni Yahwe, maana ni mwema, na uaminifu wa agano lake wadumu milele.
«Danket dem Herrn, denn er ist gütig, denn seine Gnade währt ewig!»
2 Waseme hivi waliokombolewa na Yahwe, wale aliowaokoa toka mkononi mwa adui.
So sollen sagen die Erlösten des HERRN, die er aus der Hand des Feindes erlöst
3 Yeye amewakusanya kutoka nchi za kigeni, kutoka mashariki na magharibi, kutoka kaskazini na kusini.
und die er aus den Ländern zusammengebracht hat, vom Aufgang und vom Niedergang, von Mitternacht und vom Meer,
4 Walitanga-tanga janwani katika njia ya nyika hawakuona mji wa kuishi.
die irregingen in der Wüste, auf ungebahntem Weg und keine Stadt fanden, wo sie wohnen konnten,
5 Kwa sababu walikuwa na njaa na kiu, walikata tamaa kutokana na uchovu.
hungrig und durstig, daß ihre Seele in ihnen verschmachtete.
6 Kisha walimuita Yahwe katika shida yao, naye aliwaokoa toka katika dhiki yao.
Da schrieen sie zum HERRN in ihrer Not, und er rettete sie aus ihren Ängsten
7 Aliwaongoza kupitia njia ya moja kwa moja waweze kwenda mjini kuishi humo.
und führte sie auf den rechten Weg, daß sie zu einer bewohnten Stadt gelangten,
8 Oh ili watu wamsifu Yahwe kwa ajili ya uaminifu wa agano lake na kwa mambo ya ajabu aliowatendea wanadamu!
die sollen dem HERRN danken für seine Gnade und für seine Wunder an den Menschenkindern,
9 Maana hutosheleza shauku za walio na kiu, na hamu ya wale wenye njaa yeye huwashibisha kwa mambo mema.
daß er die durstige Seele getränkt und die hungernde Seele mit Gutem gesättigt hat!
10 Baadhi walikaa katika giza na uvuli wa mauti, walifungwa katika mateso na minyororo.
Die in Finsternis und Todesschatten saßen, gebunden in Elend und Eisen,
11 Hii ni kwa sababu walikuwa wameliasi neno la Mungu na walikataa maelekezo ya Aliye Juu.
weil sie den Geboten Gottes widerstrebt und den Rat des Höchsten verachtet hatten,
12 Aliinyenyekesha mioyo yao kupitia magumu; walipata mashaka na hakukuwa na mmoja wa kuwasaidia.
so daß er ihr Herz durch Strafe beugte, daß sie dalagen und ihnen niemand half.
13 Kisha wakamwita Yahwe katika shida yao, naye akawatoa katika dhiki yao.
Da schrieen sie zum HERRN in ihrer Not, und er rettete sie aus ihren Ängsten,
14 Aliwatoa gizani na kwenye uvuli wa mauti na kuvunja vifungo vyao.
und führte sie aus Finsternis und Todesschatten heraus und zerriß ihre Bande,
15 Oh ili watu wamsifu Yahwe kwa ajili ya uaminifu wa agano lake na kwa mambo ya ajabu aliyoyatenda kwa wanadamu!
die sollen dem HERRN danken für seine Gnade und für seine Wunder an den Menschenkindern,
16 Kwa maana amevunja malango ya shaba na kukata mapingo ya chuma.
daß er eherne Türen zerbricht und eiserne Riegel zerschlägt!
17 Walikuwa wapumbavu katika njia zao za uasi na kuteswa kwa sababu ya dhambi zao.
Die Toren, die wegen ihrer Übertretung und um ihrer Missetaten willen geplagt wurden,
18 Walipoteza hamu yao ya kula chakula chochote, na waliyakaribia malango ya kifo.
daß ihrer Seele vor aller Nahrung ekelte und sie nahe waren den Pforten des Todes.
19 Kisha walimlilia Yahwe katika shida yao, naye akawatoa katika dhiki yao.
Da schrieen sie zum HERRN in ihrer Not, und er rettete sie aus ihren Ängsten.
20 Alituma neno lake na likawaponya, na akawaokoa kutoka katika uharibifu wao.
Er sandte sein Wort und machte sie gesund und ließ sie ihren Gräbern entrinnen,
21 Oh ili watu wamsifu Yahwe kwa ajili ya uaminifu wa agano lake na kwa mambo ya ajabu aliyoyatenda kwa wanadamu!
die sollen dem HERRN danken für seine Gnade und für seine Wunder an den Menschenkindern,
22 Na watoe dhabihu ya shukrani na kutangaza matendo yake kwa kuimba.
sollen ihm Dankopfer bringen und seine Taten jubelnd erzählen!
23 Baadhi husafiri baharini katika meli na kufanya biashara juu ya bahari.
Die in Schiffen sich aufs Meer begaben und Handel trieben auf großen Wassern,
24 Hawa huona matendo ya Yahwe na maajabu yake baharini.
die des HERRN Werke sahen und seine Wunder auf hoher See,
25 Kwa maana aliamuru na alivumisha upepo wa dhoruba ambao uliyainua juu mawimbi ya baharini.
wenn er sprach und einen Sturmwind erregte, der die Wellen in die Höhe warf,
26 Walipanda juu mawinguni na kushuka vilindini. Nafsi zao ziliyeyuka katika dhiki.
daß sie emporfuhren gen Himmel und hinabfuhren zur Tiefe und ihre Seele vor Angst verging;
27 Waliyumba-yumba na kupepesuka kama walevi na hawakujua la kufanya.
daß sie wirbelten und schwankten wie Trunkene, und alle ihre Weisheit dahin war.
28 Kisha walimlilia Yahwe katika shida yao, naye akawatoa katika dhiki yao.
Da schrieen sie zum HERRN in ihrer Not, und er führte sie heraus aus ihren Ängsten;
29 Aliituliza dhoruba, na mawimbi yakatulia.
er stillte den Sturm, daß er schwieg und die Wellen sich beruhigten;
30 Ndipo walifurahia kwa sababu bahari ilikuwa shwali, na aliwaleta kwenye bandari waliyoitamani.
und jene wurden froh, daß sie sich legten; und er führte sie an das erwünschte Gestade,
31 Oh, ili watu wamsifu Yahwe kwa ajili ya uaminifu wa agano lake na kwa mambo ya ajabu aliyowatendea wanadamu!
die sollen dem HERRN danken für seine Gnade und für seine Wunder an den Menschenkindern
32 Wamtukuze yeye katika kusanyiko la watu na wamsifu yeye katika baraza la viongozi.
und sollen ihn erheben in der Versammlung des Volkes und im Kreise der Ältesten ihn rühmen!
33 Aligeuza mito ikwa jangwa, chemchem ya maji ikawa nchi kame,
Er machte Ströme zur Wüste und ließ Wasserquellen vertrocknen;
34 na nchi ya matunda mengi ikawa nchi isiyozaa kwa sababu ya uovu wa watu wake.
fruchtbares Land wurde zur Salzwüste wegen der Bosheit derer, die es bewohnten.
35 Aligeuza jangwa likawa ziwa la maji na nchi kame ikawa chemchem ya maji.
Er machte aber auch die Wüste zum Wasserteich und dürres Land zu Wasserquellen.
36 Aliwakalisha huko wenye njaa, nao walijenga mji na kuishi humo.
Und er ließ Hungrige daselbst wohnen, und sie gründeten eine bewohnte Stadt;
37 Walijenga mji ili kupanda mimea shambani, kupanda mizabibu, na kuleta humo mazao tele.
und sie säten Äcker an und pflanzten Weinberge und hatten von den Früchten einen schönen Ertrag;
38 Yeye huwabariki wameongezeka sana katika hesabu. Haachi mifugo yao ipungue katika hesabu.
und er segnete sie, daß sie sich stark mehrten, und auch ihres Viehs machte er nicht wenig,
39 Kisha wakapungua na kudhilika kwa dhiki na mateso.
nachdem sie vermindert worden waren und gedemütigt durch den Druck des Unglücks und Kummers,
40 Akawamwagia viongozi dharau na akawafanya wazunguke katika jangwa, mahali pasipo na njia.
als er Verachtung auf die Fürsten goß und sie irregehen ließ in unwegsamer Wildnis;
41 Lakini aliwalinda wahitaji dhidi ya mateso na kujali kwa ajili ya familia yake kama kundi la kondoo.
aber er erhob den Armen aus dem Elend und machte die Geschlechter wie Schafherden.
42 Wenye haki wataona hili na kufurahi, na uovu wote utaona na kufunga kinya chake.
Die Redlichen sollen es sehen und sich freuen, und alle Bosheit soll ihr Maul verschließen!
43 Yeyote mwenye hekima anapaswa kuyaangalia haya na kutafakari juu ya matendo ya uaminifu wa agano la Yahwe.
Wer weise ist, der beobachte solches und merke sich die Gnadenerweisungen des HERRN!